Pages


Home » » AJALI YAUA WATOTO WAWILI WANANCHI WAFUNGA BARABARA.

AJALI YAUA WATOTO WAWILI WANANCHI WAFUNGA BARABARA.

Kamanga na Matukio | 05:50 | 0 comments
 Miili ya watoto Timotheo Omary(5) na Thadeo Bryston Malila(5) waliofariki kupitia ajali iliyotokea Kijiji cha Imezu,Kata ya Inyala Mkoani Mbeya
 
 Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Dk. Norman Sigalla akiwa na Meneja wa TANROADS mkoani Mbeya wakibadilishana mawazo namna ya kuweka matuta eneo la Imezu lililokithiri kwa ajali.
 Baadhi ya wananchi wa Imezu wakisukuma gogo kupeleka barabarani kwa ajili ya kufunga barabara kufuatia ajalihiyo.
 Mwandishi wa habari Bwana Charles Mwaipopo akiwa eneo la tukio.
Na Ezekeil Kamanga Mbeya
Matukio ya ajali yameendelea kuandamwa Mkoa wa Mbeya  baada ya wananchi  wa Kijiji cha Imezu  kata ya Inyala  wilaya ya Mbeya Vijijini  jana kulazimika kufunga bara bara ya  Mbeya  Dar es Salaam kwa masaa sita baada ya kutokea ajali iliyoua watoto  wawili wa chekechea wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka mitano mpaka sita wanafunzi wa shule  ya msingi Imezu.

Imeelezwa kuwa wananchi hao  waliamua kuchukua  uamuzi huo  baada ya kuchoshwa na ahadi za serikali kupitia wakala wa bara bara ambazo zimekuwa hazitekelezwi  katika eneo hilo la la shule  ya msingi Imezu na kuendelea kukatiza uhai wa watu.

Akizungumza na gazeti hili Mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Imezu Bw. Seif John alisema kuwa tukio la kufungwa kwa bara bara hiyo limetokea majira ya saa 1.15 asubuhi baada ya watoto hao kugongwa na gari aina ya Lori la mafuta  yenye namba T 698 BVY lenye tela namba T 798 BVA lililokuwa likiendeshwa na dereva Dominick Anton Mwakalundwa(34) likitokea Mbeya  kwenda Mkoani Iringa liligonga watoto  hao waliokuwa pembeni ya bara bara wakitoka shule.

Bw. John alisema kuwa baada ta tukio hilo kutokea wananchi walijaa eneo la ajali  na kuanza kufunga  bara bara kwa kutumia magogo na mawe  ili kuzuia magari yasipite eneo hilo kwa lengo la kushinikiza serikali kuweka matuta ili kuzuia ajali.

“Unajua  haya matukio  ya ajali yamekuwa yakitokea mara kwa mara katika eneo hili la shule  ambapo mpaka sasa zaidi  ya watu 30 wameshafariki dunia  kwa ajali kama hizi, sasa  hiii hali tumechoka kwani zimekuwa ahadi tu bila utekelezaji wowote tunashindwa kuelewa kinachofanya wasiweke matuta nini  wakati uwezo upo, wanasubiri mpaka madhara makubwa yatokee zaidi ya hili “alihoji mwananchi huyo.

Hata hivyo baada ya tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Dkt. Norman  Sigalla  aliwaomba wananchi  kufungua bara bara wakati serikali  kwa kushgirikiana na wakala wa bara bara (TAN ROADS) ikiwa inaweka utaratibu  wa kuweka matuta hayo haraka iwezekanavyo.

“Nimesikia kilio chenu kwani hata mimi msiba huu umenigusa kwani naliagiza jeshi la polisi mKoani hapa kuwachukulia hatua  kali madereva wataoendesha  magari kwa mwendo kasi  na kwamba watozwe faini na adhabu kali ambayo itawafanya wawe na nidhamu  na askari wasiwe marafiki wa madereva”alisema Mkuu huyo wa wilaya.

Aidha  wananchi hao walisema kuwa wamechoshwa na  mwendo kasi wa madereva katika eneo hilo kwani na kuongeza kuwa ajali hizo zimekuwa zikipoteza nguvu kazi ya Taifa kwa kiasiu kikubwa.

Hata hivyo baada ya tukio hilo kutokea dereva  wa gari iliyosabisha ajali hiyo alienda kujisalimisha mwenye katika kituo kidogo cha Inyala  kwa usalama kutokana na wananchi kuwa na hasira.

Akizungumza katika  eneo la tukio Diwani wa kata ya Inyala Bw. Libareto Mwalingo alisema kuwa ameandika barua  kwa wakala wa bara bara mara nyingi  kuomba kuwekewa  matuta  hayo  bila mafanikio  yeyote huku  matukio hayo yakiendelea kumaliza wananchi wa eneo hilo.

Baadhi ya wananchi wa enbeo hilo walisema kwamba kama serikali imeshindwa  kuweka matuta  basi ihamishe  shule kwani watoto walio wengi wanaosoma shule hiyo wanatoka upande wa pili  wa bara bara ambao unawalazimu kuvuka bara bara.

Miili ya watoto hao  imepelekwa katika hospitali ya Inyala kwa uchunguzi  ili iweze kukabidhiwa kwa ndugu zao kwea maziko ambapo watoto hao wote ni wa kiume.

Hata hivyo watoto waliofariki wametambuliwa kwa majina ya Timotheo Omary(5) na Thadeo Bryston Malila(5) wote ni wanafunzi wa awali.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger