Pages


Home » » ANGALIZO TUNAOMBA RADHI KWA PICHA KWA PICHA HIZI ZA KUTISHA, UKATILI ULIOKITHIRI MAUAJI YA WATU WATATU MKOANI MBEYA.

ANGALIZO TUNAOMBA RADHI KWA PICHA KWA PICHA HIZI ZA KUTISHA, UKATILI ULIOKITHIRI MAUAJI YA WATU WATATU MKOANI MBEYA.

Kamanga na Matukio | 02:40 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya
 *Wawili wauawa na kisha kuchomwa moto akiwemo Askari Magereza.
Askari magereza  Abel Mwakajonga(24) na nduguye Ezekiel Gambi(30) mkazi wa Ukwile, Kata ya Mlangali Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya, wamefikwa na mauti  siku ya Jumamosi Desemba 8 mwaka huu baada ya kukodi bodaboda kutoka Mlowo kuelekea Mlangali kwa ajili ya kumkamata mtuhumiwa wa mauaji Bwana Laiton Ngonya.

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kumuua baba yao marehemu Salumu Gambi, mnamo Novemba  4 mwaka huu na kuzikwa siku inayofuata katika Kijiji cha Chizumbi mpakani mwa Wilaya ya Ileje na Mbozi .

Kwa mujibu wa maelezo ya mdogo wa marehemu Ezekia, bwana Godfrey Gambi(26) amesema kulikuwepo na mawasiliano baina ya simu baina ya Zemu Kayila ambaye ni dereva bodaboda iliyokodiwa na marehemu hao na Bwana Ngonya, ambapo baada ya kufika kijijini hapo marehemu walipotaka kumkamata  mtuhumiwa alipiga yowe akidai watu hao(marehemu) ni wezi wa pikipiki ndipo wananchi walianza kuwapiga kwa vitu vyenye ncha kali yakiwemo mapanga na visu hadi kuwasababishia mauti.

Wananchi hao hawakuishia hapo waliwavua nguo na kuwateketeza kwa moto na miili kuachwa eneo la tukio, huku uongozi wa kijiji hicho kutokuwa na taarifa.

Aidha Mwenyekiti wa Kijiji cha Ukwile Bwana Osia Mtawa, amesema baada ya mauaji hayo alipata taarifa na kisha kutoa taarifa Polisi Wilaya ya Mbozi ambapo walifika majira ya saa 12:00 jioni na kuichukua miili ya marehemu  hadi Hospitali ya wilaya hiyo kwa ajili ya uchunguzi uliofanywa na Daktai Makala siku ya Jumapili Desemba 9 mwaka huu.

Mwili wa marehemu Ezekia Gambi ulifanyiwa uchunguzi majira ya saa 5:43 na mwili wa Askari Abeli Mwakajonga saa 5:51 na taarifa kukabidhiwa Polisi.

Hata hivyo ndugu wa marehemu walikabidhiwa miili ya marehemu hao saa nane baada ya kupata kibali cha Polisi ambapo marehemu Mwakajonga amezikwa katika Kijiji cha Mbebe wilaya ya Ileje na mwili wa marehemu Gambi umezikwa Kijiji cha Ukwile wilaya ya Mbozi.

Wakati huo huo mauaji haya yamekuja siku moja na tukio la kuuawa kikatili kwa Afisa mstaafu wa Usalama wa Taifa Mzee Joseph Mwasokwa, aliyeuawa nje ya nyumba yake eneo la Block T mkoani hapa kuwa mashakani licha ya Kamanda wa Jeshi la polisi mkoani Diwani Athuman kufanya juhudi kubwa ya kupambana na uhalifu .

Kamanda huyo ametoa wito kwa yeyote atakayetoa taarifa za kupatikana watu waliojichukulia sheria mkononi na waliohusika na mauaji ya Afisa Usalama ili kufanya mkoa kuwa na hali ya amani na utulivu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger