Pages


Home » » WANANCHI SONGWE MBEYA WAANDAMANA KUTAKA MATUTA

WANANCHI SONGWE MBEYA WAANDAMANA KUTAKA MATUTA

Kamanga na Matukio | 19:06 | 0 comments









 SISI NI WANAFUNZI, WAZAZI NA WENZETU WAMEPOTEZA MAISHA HAPA KWA KUGONGWA INGAWA KUNA PUNDA MILIA LAKINI MADEREVA HAWAJALI KAULI ILE YA KIBURI SI MAUNGWANA


 JAMANI SISI NI VIONGOZI WA WILAYA HII, TUNAOMBA MTUSIKILIZE



 NAITWA SIMON MKINA KAIMU MENEJA WA TANROAD MBEYA, KWA LEO HAIWEZEKANI LAKINI TUTAJENGA MATUTA




BAADHI ya wananchi wa kijiji cha Songwe wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya wameandamana tangu asubuhi kwa ajili ya kuishinikiza Serikali kuweka matuta eneo hilo baada ya kutokea ajali za mara kwa mara eneo hilo.

Wamesema kuwa hatua hiyo wameifikia baada ya kushuhudia ajali mbaya jana ambapo aligongwa mtoto Ezekiel Mwaula wa shule ya Msingi Saruji.

Uongozi wa wilaya ya Mbeya pamoja na Tanroad mkoa wa Mbeya wakiongozwa na Injinia Simon Mkina wamefika kuwaomba wananchi kutuliza hasira, hatimaye wananchi wamekubali kwa kuchagua viongozi watano ii kufuatilia 
utekelezaji.

Kwa hisani ya Kalulunga
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger