Pages


Home » » ALIYEUAWA MBEYA JK AMTUMA KAKA YAKE MAZISHI YA OFISA USALAMA ALIYEUAWA MBEYA

ALIYEUAWA MBEYA JK AMTUMA KAKA YAKE MAZISHI YA OFISA USALAMA ALIYEUAWA MBEYA

Kamanga na Matukio | 04:04 | 0 comments

MAZISHI ya aliyekuwa ofisa Usalama wa Taifa (mstaafu) mkoa wa Mbeya RSO Joseph Nelson Mwasokwa, aliyeuwawa usiku wa kuamkia Desemba 9, mwaka huu Jijini Mbeya, yamefanyika katika Kijiji cha Ibungu wilayani Kyela mkoani Mbeya.
 Marehemu pia alikuwa mwanachama wa Timu ya soka ya Yanga.
 Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Ndg. Joseph Mbilinyi(kushoto) na Mwenyekiti wa Mtaa wa Block T Ndg. Majembe(kulia). Mtaa wa Block T ndiko alikokuwa akiishi marehemu.
Kaka wa rais Kikwete Selemani Kikwete akinigia wilayani kyela kwenye mazishi ya marahamu mzee mwasokwa
Aliyekuwa mkuu wa mkoa mbeya Mwakipesile akiongea na mzee Mwambulukutu kwenye mazishi ya marehemu Mwasokwa
Waombolezaji 

Katika mazishi hayo, Rais Jakaya Kikwete aliwakilishwa na kaka yake Selemen Kikwete ambaye pia alipata nafasi ya kutoa pole kwa waombolezaji ambao hawakuruhusiwa kuuona mwili wa marehemu bali kilichoruhusiwa kuangaliwa ni picha yake iliyokuwa juu ya jeneza.
Mbali na Seleman Kikwete, viongozi mbalimbali nwalihudhuria msiba huo akiwemo Mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wa Taifa Tanzania Ndugu Othuman, aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Mbeya mstaafu John Mwakipesile na viongozi kadhaa waandamizi wa Serikali.
Marehemu Mwasokwa akatwa na kitu chenye ncha kali kisogoni ambako wauaji ambao hawajajulikana walifanya kitendo hicho kisha kuulaza mwili wake kifudifudi nje ya geti la nyumba yake eneo la Block T jijini Mbeya.

Taarifa za Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, zimesema kuwa wauaji wanaonekana kuwa walitumia panga ambapo marehemu alikutwa na majereha makubwa sehemu za shingoni, kichwani, mabegani na mkono wa kushoto.
Kwa hisani ya Kalulunga
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger