Pages


Home » » WANAWAKE WATAKIWA KUWA NA DAFTARI LA KUMBUKUMBU LA BIASHARA,

WANAWAKE WATAKIWA KUWA NA DAFTARI LA KUMBUKUMBU LA BIASHARA,

Kamanga na Matukio | 01:27 | 0 comments
Na Ester Macha.
 WANAWAKE Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya wametakiwa kuwa na daftari la kumbu kumbu  la biashara ambazo wanazifanya kila siku  ili liweze kuwapa tathimini  ya biashara wanazofanya ambayo itawasaidia kusonga mbele kimaisha na kuachana na dhana ya kuwa tegemezi kwa waume zao.

Imeelezwa kuwa baadhi ya wanawake wamekuwa wakishindwa kuwa na tathimini nzuri nzuri ya fedha zao za biashara kutokana na kuwa na nidhamu mbaya ya matumizi ya fedha wanazozipata katika biashara zao.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati wa Kongamano la mwanamke jitambue   lilofanyika katika ukumbi wa Chinga Wilayani Mbarali ,na Mwakilishi wa Shirika la Elimisha ambalo linajishughulisha na masuala ya watoto yatima,wanawake, pamoja na watoto wanaoishi katika mazingira magumu Bw. Festo Sikagonamo  wakati wa kuwasilisha mada ya ujasiliamali kwa wanawake.

Bw. Sikagonamo alisema kuwa kitendo cha wanawake wajasilimali waliopo mijini na vijijini kuwa na  daftari la kumbu kumbu  la bidhaa mbali mbali wanazouza kutasaidia kukuza bishara zao na hatimae kuwa na nidhamu nzuri ya matumizi fedha zao .

“Kwa utaratibu huu ikifika mwisho wa mwezi au mwaka  mwanamke ataweza kujua hesabu zake kwa uhakika kuwa fedha hiyo afanyie  kitu gani cha msingi kwasababu tayari atakuwa kwenye msingi mzuri wa biashara na atakuwa amepata faida kubwa, na nyie wanawake mliofanikiwa kupata elimu hii ya ujasiliamali jitahidini kufika maeneo vijijini kuwapa elimu  hiyo “alisema Mwakilishi huyo wa Shirika la Elimisha.

Hata hivyo alisema kuwa Tofauti  ya miongoni mwa wanawake nchini  wamekuwa hawana kanuni  nzuri  za kibiashara kwani  katika matumizi yao ambayo wameweka  yanakuwa hayatoshi  hivyo ni jukumu kwa kila mwanamke kuongeza juhudi  ili kufanikisha kile alichoshindwa lakini si kutoa fedha ambayo hajapangia matumizi.

Kwa upande wa Mratibu wa Kongamano hilo Bibi.Groly Komba alisema kuwa  lengo la kongamano hilo ni  ni kutoa ufahamu kwa wanawake  kuhusiana na  masuala ya kijamii na kiuchumi, malezi bora  kwa watoto, sheria ya ndoa na mirathi,pamoja na masuala ya  ukimwi ambayo ni  maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Hata Hivyo Bibi. Komba alisema kuwa  kitu kingine ambacho kilizungumziwa  katika kongamano hilo ni  suala la uchumi ambalo ni ujasiliamali ,vikoba, kwa  kuweka akiba ikwa kutumia vikoba  hivyo kwa wanawake .

“Lakini pia tumeanza mkakati wa  na  mtandao  wa wanawake wilayani Mbarali kwa kuwaweka wanawake pamoja ili kutafuta  wanawake wenye taaluma mbali mbali ambao wataweza kutoa elimu za ujasiliamali kwa wanawake”alisema Mratibu huyo.

Mmoja baadhi ya wanawake walioshiriki Kongamano hilo Bi . Elizabeth  Saro alisema kuwa kongamano hilo lilikuwa zuri  kwani wamejifunza mambo mengi  hasa ujasiliamali, matumizi ya fedha, malezi ya watoto wao.

Aidha alisema kuwa kongamano hilo limeweza kuwatoa walipo na kufika sehemu fulani  kwani pia wameweza kujifunza  suala la maambukizi kutoka mama kwenda kwa mtoto jinsi  ya kijizuia ili mtoto asiweze kuambukizwa na ugonjwa huo.

Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger