Pages


Home » » HABARI KAMILI KUHUSU UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA SONGWE MBEYA WAANZA KUTUMIKA NDEGE ZAIDI YA TATU ZATUA

HABARI KAMILI KUHUSU UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA SONGWE MBEYA WAANZA KUTUMIKA NDEGE ZAIDI YA TATU ZATUA

Kamanga na Matukio | 02:31 | 0 comments

Mwandishi wa habari kutoka Kituo cha redio kinachofahamika kutoka Nyanda za Juu Kusini Bomba FM na Blogu ya Kamanga na Matukio Ndg. Ezekiel Kamanga akishuka katika ndege katika uzinduzi wa uwanja huo wa Ndege wa kimataifa uliopo Songwe Mkoani Mbeya. 
Brandy Nelson,Mbeya
HATIMAYE  Ndege ya  kwanza ya abiria  imetua  katika Uwanja wa kimataifa wa Songwe rasmi leo baada ya miaka 11 ujenzi wake ambao  tayari umekamilika na kugharimu kiasi cha sh.100 bilioni.

Akizungumza  baada ya kutua ndege hiyo  Kaimu Mkurugenzi wa malamalaka ya Viwanja vya ndege Tanzania (TAA) Seleman  Seleman alisema kuwa tayari uwanja wa kimataifa wa Songwe umekamilika na dunia nzima inataarifa ya  kukamilika kwa uwanja huo.

Alisema kuwa kutokana na kukamilika kwa uwanja huo tayari ofisi za mamalaka hiyo imeshahamia katika uwanja huo na kuanza shughuli zake rasmi leo ambapo uwanja wa zamani  umefungwa rasmi hakuna ndege yoyote itakayoweza kutua katika uwanja huo.

“Kimeanzisha historia mpya kwani dunia inafahamau kwa asasa kwamba uwanja wa kimataiafa wa Songwe upo wazi umekamilika na umeanza kutumika rasmi leo”alisema

Alisema kuwa Uwanja wa songwe wa kimataifa ni  kati ya  viwanja vikubwa viwili  kujengwa  baada ya uhuru ukitanguliwa na uwanja wa  mkoa wa Kilimanjaro kwani viwanja vingine vimekuwa vikifanyiwa marekebisho.

Kwa upande wake kaimu mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Mkuu wa Wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro alisema aliwataka wananachi wa Mkoa wa Mbeya kujiandaa kutumia uwanja huo kwa kuongeza kipato chao na kuinua uchumi wa Mkoa.

Alisema kuwa Wakazi wa Mbeya wanaopaswa kuzalisha kwa wingi maua na matunda ili kutumia vizuri uwanja huo ili uchumi wa mkoa uweze kukua “tusiutumie uwanja huu kwa lengo la kusafiria pekee”alisema

“Uwanja wa Songwe ni fulsa muhimu  kwa wakazi wa mkoa wa Mbeya na mikoa jirani kwani utaweza kuwasaidia katika kuongeza pato la mtu mmoja mmoja na taiafa kwa ujumla kutokana na uwanja huo kuwa wa kimataifa ambapo shughuli mbali mbali za  kiuchumi zitafanyika kutokana na uwanja huo”alisema

Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger