Pages


Home » » Rais Kikwete, Serikali haliifanyii makusudi suala la kutoongeza mishahara kwa wafanyakazi.

Rais Kikwete, Serikali haliifanyii makusudi suala la kutoongeza mishahara kwa wafanyakazi.

Kamanga na Matukio | 03:12 | 0 comments

MHESHIMIWA RAISI AKIHUTUBIA MAELFU YA WANANCHI NA WAFANYAKAZI WALIOKUSANYIKA UWANJANI.
Na Ezekiel Kamanga, ,Mbeya
Rais Jakaya Kikwete amelitaka shirikisho la vyama vya wafanyakzi nchini (Tucta) kutambua kuwa suala la kutoongeza mishahara kwa wafanyakazi serikali hailifanyii makusudi suala hilo .
 
Amesema  uongezaji wa mishahara kwa wafanyakazi linaendana ukubwa wa bajeti yenye hasa katika ukusanyaji wa kodi .
 
Raisi Kikwet amesema hayo leo jijini Mbeya katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakzi Duniani Mei Mosi ambapo kitifa imefanyika mkoanui humo katika uwanja wa kumbukumbu ya sokoine na kuhudhuliwa na baadhi ya viongozi mbalimbali wakiwemo mawaziri na mabarozi.
 
Katika hotuba yake Rais Kikwete ameelezea niya ya serikali katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazo wakabili wafanyakazi nchi likiwepo suala la mishahara na tozo kubwa ya kodi.
 
Rais Kikwete amesema kuwa nivema shirikisho hilo liktambua kuwa serikali imekuwa ikifanya kila jitihada katika kuendelea ku boresha maisha ya wafanyakzi nchini.
 
Amesema katika mwaka ujao wa fedha serikali itaongeza kima cha chii cha mishahara hasa kutokana kuongezeka kwa ukusanyaji wa mapato  kutoka zaidi ya shilingi bilioni 5 kwa mwaka hadi bilioni 6 ambazo kwa asilimia kubwa zimetengwa katika kuongeza mishahara ya wafanyakazi kwa asailimia 44.
 
Hata  hivyo Kikwete amesema  tamko rasmi la kuongeka kwa kima hicho cha chini cha mishahara ya wafanyakazi kitatolewa na waziri wa fedha wakati akiwasilisha bajeti yake  katika vikao vya bunge Dodoma .
 
 
Katika suala la punguzo la kodi kwa wafanyakazi hao Rais Kikweta amesema kuwa katika mwaka 2009/2010 serikali ilipunguza tozo ya kodi kutoka asilimia 18 hadi 15 ambapo  kwa mwaka 2011/2012 punguzo la kodi lilikiwa asilimia 14 hivyo bado  serikali inaendelea kulipunguza tatizo hilo.
 
Hata hivyo Kikwete amesema anatambua kuwa zipo changamoto nyingi zinazo wakabili wafanyakazi hao lakini ameahidi  kuendelea kuzifanyia kazi  pamoja na kukaa na viongozi wao katika kuzungumzia mbalimbali yanayo lihusu shiriksho hilo .
 
 
Wakati huo Mheshimiwa  Raisi amewatoa kwa wafanayakzi watakao staafu kuwa suala la kupata fao lao la kustaafu litatolewa licha ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali zinazoukabili mfuko huo wa hifadhi ya jamii (SPF)
 
Amesema  serikali imejiwekea mkakati wa kuhakisha inaweka kiasi cha shilingi bilioni 50 kila mwaka ili kuhakikisha kila atakye staafu anapatiwa haki yake bila kuchelewa.
 
Pia ametoa wito  wa mifuko ya hifadhi ya kijamii njini kucha tabia ya kuwalazimisha wafanyakazi hao kujiunga na mifuko hiyo kwani kinyume cha taratibu na sheria ya mifuko hiyo.
 
Katika saula la amani Raisi Jakaya Kikwte Pia amewataka wananchi Mkoani humo na watanzania kwa ujumla kuendelea kuilinda amani iliyopo kwani madahara ya kutokewaka kwa amani ni makubwa hivyo amewataka kungana kwa pamoja kuilinda amani hiyo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger