Pages


Share to TwitterShare to Facebook WATANZANIA WATAKIWA KUWA WABUNIFU KATIKA UFANYAJI KAZI KWA BIDII.

Kamanga na Matukio | 01:11 | 0 comments
Na Esther Macha, Mbeya
WATANZANIA wametakiwa kuacha kumtafuta mchawi wa hali duni ya maisha yao na kulalamika hali duni ya maisha na badala yake wawe wabunifu,wajitathmini na kufanyakazi kwa bidii na maarifa ili waweze kujipatia kipato na maendeleo ya familia,jamii na taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bw.Abbas Kandoro wakati akifungua mkutano wa mashauriano juu ya malengo nane ya melania katika ukumbi wa paradise,jijini Mbeya ambapo wadau kutoka mikoa ya Ruvuma,Rukwa,Njombe,Katavi na Mbeya walishiriki mkutano huo.

Aidha Bw. Kandoro ametoa  maoni yake kuwa endapo kila mtanzania atajituma katika kutafuta maisha na kuzitumia fursa zinazomzunguka,akaacha kuwa mnung’unikaji wa hali ngumu ya maisha huku amekaa kijiweni,akaacha kumtafuta mchawi kwa kila linalomsibu,akawa mchangiaji katika kuhakikisha hali ya utulivu na amani inadumishwa kwa kuheshimu misingi ya utawala bora,kasi ya kuliendeleza taifa itakuwa kubwa.

"Kwa sasa bado tunaongea sana, ‘we are talking a lot,’ninaamini mkusanyiko huu utasaidia sana kufanya tathmini ya pamoja kujuwa tulikotoka,tulipo na tunakokwenda,ninaipongeza serikali kuteuwa Taasisi ya utafiti katika Nyanja za uchumi na jamii (ESRF) ifanye kazi ya kukusanya maoni ya wadau mbalimbali,"alisema .

Alisema utekelezaji wa malengo ya millennia kwa Tanzania unatofautiana kila Mkoa na Wilaya na ametolea mfano kwenye eneo la Ukimwi,Mkoa wa Mbeya una asilimia 9.2 kwa takwimu za mwaka 2008 wakati kitaifa ni asilimia 5.7,kupunguza umaskini kitaifa imetokea asilimia 39 kwa mujibu wa takwimu za mwaka 1990 hadi asilimia 33.6 kwa takwimu za mwaka 2007.

Mkuu huyo wa Mkoa pato la mkazi wa Mbeya kwa siku ni dola 1 hadi 1.5 kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2010 ambapo katika elimu ya msingi na Sekondari ukiangalia katika uwiano wa Ke na Me wamevuka lengo kama nchi kwa asilimia 101 na 205 na kwa Mkoa wa Mbeya ni asilimia 102 na 88 ambayo kwa ujumla haijavuka lengo.

Aidha alisema lazima kukiri kuwa bado kuna changamoto katika kutokomeza umaskini wa kipato,njaa,kuboresha afya ya uzazi na huduma za maji salama pamoja na elimu.

Mkuu wa Mkoa huyo alisema kupitia warsha kutoka katika mikoa yote Tanzania, anao uhakika,ushauri na mapendekeo ya washiriki kuhusu kuamua nini kifanyike kwa siku zijazo baada ya 2015 ni muhimu sana.

Naye Dkt.John Mduma mwezeshaji ambaye ni Mhadhiri kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam alisema lengo la mashauriano hayo ni kutoa kichocheo cha mjadala wa wadau mbalimbali,kujenga taswira ya kimataifa ya hali ya baadaye kwa mapendekezo madhubuti,kuhakikisha na kusikika sauti za maskini na wasio sikika,kutambua na kuchambua masuala yatakayoathiri maendeleo,kushawishi mchakato ndani ya serikali kuu ioane na taasisi na matokeo yanayotarajiwa.

Bw.John kajiba ,Mtafiti kutoka taasisi ya utafiti wa mambo ya uchumi na jamii (ESRF-Economic and Social Research Foundation) alisema taasisi hiyo imeombwa kusimamia majadiliano hayo kwa kushirikiana na Ofisi ya rais tume ya mipango katika kanda saba na hasa katika maeneo ya Serikali za mitaa,Asasi za kiraia,watoto,wazee na wanawake wadogo.

Disemba,4,2012 kumefanyika tukio muhimu na la kihistoria kwa taifa la Tanzania kutokana na kuwa miongoni mwa nchi 50 kati ya 189 zilizochaguliwa kujadili,malengo hayo nane ya millennia katika kanda saba ambazo mahali yalipofanyika katikamabano ni kanda ya Ziwa (Mwanza),kanda ya kaskazini (Arusha),Kanda ya kati(Dodoma),kanda ya nyanda za juu (Mbeya),kanda ya kusini(Mtwara),kanda ya magharibi (Shinyanga) na kanda ya mashariki (Morogoro).

MBUNGE AWASIHI WANACHAMA WA CHADEMA KUTOINGILIA MKUTANO WA CCM JIJINI MBEYA.

Kamanga na Matukio | 01:10 | 0 comments

 Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini mheshimiwa Joseph Mbilinyi kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADE,A) akiwa juu ya gari lake, akiwasihi wakereketwa wa chama hicho kutoingilia Mkutano wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), uliofanyika eneo la Stendi ya daladala ya Kabwe Jijini Mbeya.
 Taswira kamili ya Mbunge akizungumza na wanachama wa CHADEMA
 Taswira kamili ya hatua waliyokuwa wameifikia wanachama wa CHADEMA kwa ishara ya kuwa CCM imezikwa kaburini.
Picha na Mpiga picha wetu Ezekiel Kamanga,Mbeya.

DAKTARI WA RUFAA MBEYA ATIWA MBARONI KWA MADAI YA KUPOKEA RUSHWA

Kamanga na Matukio | 01:09 | 0 comments
DAKTARI wa kitengo cha upasuaji katika Hospitali ya Rufaa Mbeya,Paul Kisabi (32), anayetuhumiwa kwa kupokea rushwa ya sh 200,000


Brandy Nelson,  Mbeya
DAKTARI  wa Hospitali ya Rufaa Mbeya Paul Ngiga amefikishwa katika mahakama ya Mkoa wa Mbeya kwa tuhuma za kushawishi na kupokea Rushwa ya sh. 200,000 kutoka kwa ndugu wa mgonjwa.

Akisoma mashitaka mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya Mkoa Mbeya Francis Keshenye Nimrodi Mafwele  akishirikiana na Joseph Mulebya alisema kuwa mshitakiwa alitenda kosa Desemba 19,2012  katika bar ya Victory.

Alisema kuwa mshitakiwa anakabiliwa na makosa mawili moja likiwa ni la kufanya ushawishi na la pili ni kupokea rushwa ya shilingi 200,000 kutoka kwa ndugu wa mgonjwa ambapo Taasisi ya kupambana na  kuzuia rushwa ilipoweka mtego wake na kufanikiwa kumkamata.

Ilidaiwa  na mwendesha mashaitaka huyo kuwa mnamo  desemba 18,2012 mshitakiwa  aliomba kiasi hicho cha fedha kutoka kwa ndugu wa mgonjwa aliyefahamika kwa jina la Meshack Mwakilambo kwa ni ya kumsaidia kumhudumia mgonjwa wake.

   Mwendesha mashitaka  Mafwele  alisema kuwa kosa hilo ni kinyume cha sheria kanuni ya adhabu  cha makosa ya jinai kilichofanyiwa marekebisho mwaka 2007 ambapo  ni kifungu cha 15 kifungu kidogo cha kwanza (a).

Hakimu wa mahakama ya haklimu mkazi Mkoa wa Mbeya Francis Keshenyi alisema mahamani kuwa dhamana ipo wazi na kwamba kesi hiyo italetwa mahakamani hapo hadi Desemba,27,2012.

Mshitakiwa baada ya kusisomewa mashitaka hayo alikanusha kutenda kosa hilo na mshitakiwa yupo nje baada ya kutimiza masharti ya dhamana  na alidhaminiwa na mdhamini mmoja kwa gharama ya sh 500,000.

PICHA YA MLINZI ALIYEUAWA KIKATILI.

Kamanga na Matukio | 01:41 | 0 comments
Mlinzi binafsi Simon Mwambene(45) Mkazi wa Kijiji cha Matula, Mbozi Mission Kata ya Magamba Wilaya ya Mbozi, Mkoani Mbeya, ameuawa na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi alipokuwa lindo Desemba 13 mwaka huu majira ya saa 8:15 usiku alipokuwa analinda maduka 9 yaliyopo kijijini hapo yanayomilikiwa na Bwqana Frank Tenson, Mgala, Tweve, Sosten Kibona, Raphael Kisunga, Kamika Simbeye, Crispin Ndabila, Gody Mahenge, Anthon Mwazembe na Samwel Ndabila (Picha na Ezekiel Kamanga).

PICHA YA KIUMBE WA AJABU ALIYEZALIWA MKOANI MBEYA.

Kamanga na Matukio | 01:28 | 0 comments
Kiumbe wa ajabu azaliwa Mbeya, Viungo vyake vyazua gumzo macho yake yako katikati ya paji la Uso akosa Pua ila ana mdomo..!!!
 Mama aliyejifungua kiumbe wa ajabu Bi. Melina Wilson mwenye umri wa miaka 17.
Baba mzazi wa kiumbe wa ajabu Bwana Emmanuel Mbukwa mwenye umri wa miaka 24.(Picha na Ezekiel Kamanga, Mbeya.)

WANAWAKE WATAKIWA KUWA NA DAFTARI LA KUMBUKUMBU LA BIASHARA,

Kamanga na Matukio | 01:27 | 0 comments
Na Ester Macha.
 WANAWAKE Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya wametakiwa kuwa na daftari la kumbu kumbu  la biashara ambazo wanazifanya kila siku  ili liweze kuwapa tathimini  ya biashara wanazofanya ambayo itawasaidia kusonga mbele kimaisha na kuachana na dhana ya kuwa tegemezi kwa waume zao.

Imeelezwa kuwa baadhi ya wanawake wamekuwa wakishindwa kuwa na tathimini nzuri nzuri ya fedha zao za biashara kutokana na kuwa na nidhamu mbaya ya matumizi ya fedha wanazozipata katika biashara zao.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati wa Kongamano la mwanamke jitambue   lilofanyika katika ukumbi wa Chinga Wilayani Mbarali ,na Mwakilishi wa Shirika la Elimisha ambalo linajishughulisha na masuala ya watoto yatima,wanawake, pamoja na watoto wanaoishi katika mazingira magumu Bw. Festo Sikagonamo  wakati wa kuwasilisha mada ya ujasiliamali kwa wanawake.

Bw. Sikagonamo alisema kuwa kitendo cha wanawake wajasilimali waliopo mijini na vijijini kuwa na  daftari la kumbu kumbu  la bidhaa mbali mbali wanazouza kutasaidia kukuza bishara zao na hatimae kuwa na nidhamu nzuri ya matumizi fedha zao .

“Kwa utaratibu huu ikifika mwisho wa mwezi au mwaka  mwanamke ataweza kujua hesabu zake kwa uhakika kuwa fedha hiyo afanyie  kitu gani cha msingi kwasababu tayari atakuwa kwenye msingi mzuri wa biashara na atakuwa amepata faida kubwa, na nyie wanawake mliofanikiwa kupata elimu hii ya ujasiliamali jitahidini kufika maeneo vijijini kuwapa elimu  hiyo “alisema Mwakilishi huyo wa Shirika la Elimisha.

Hata hivyo alisema kuwa Tofauti  ya miongoni mwa wanawake nchini  wamekuwa hawana kanuni  nzuri  za kibiashara kwani  katika matumizi yao ambayo wameweka  yanakuwa hayatoshi  hivyo ni jukumu kwa kila mwanamke kuongeza juhudi  ili kufanikisha kile alichoshindwa lakini si kutoa fedha ambayo hajapangia matumizi.

Kwa upande wa Mratibu wa Kongamano hilo Bibi.Groly Komba alisema kuwa  lengo la kongamano hilo ni  ni kutoa ufahamu kwa wanawake  kuhusiana na  masuala ya kijamii na kiuchumi, malezi bora  kwa watoto, sheria ya ndoa na mirathi,pamoja na masuala ya  ukimwi ambayo ni  maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Hata Hivyo Bibi. Komba alisema kuwa  kitu kingine ambacho kilizungumziwa  katika kongamano hilo ni  suala la uchumi ambalo ni ujasiliamali ,vikoba, kwa  kuweka akiba ikwa kutumia vikoba  hivyo kwa wanawake .

“Lakini pia tumeanza mkakati wa  na  mtandao  wa wanawake wilayani Mbarali kwa kuwaweka wanawake pamoja ili kutafuta  wanawake wenye taaluma mbali mbali ambao wataweza kutoa elimu za ujasiliamali kwa wanawake”alisema Mratibu huyo.

Mmoja baadhi ya wanawake walioshiriki Kongamano hilo Bi . Elizabeth  Saro alisema kuwa kongamano hilo lilikuwa zuri  kwani wamejifunza mambo mengi  hasa ujasiliamali, matumizi ya fedha, malezi ya watoto wao.

Aidha alisema kuwa kongamano hilo limeweza kuwatoa walipo na kufika sehemu fulani  kwani pia wameweza kujifunza  suala la maambukizi kutoka mama kwenda kwa mtoto jinsi  ya kijizuia ili mtoto asiweze kuambukizwa na ugonjwa huo.

Share to TwitterShare to Facebook WAZAZI BADO WAENDELEA NA DHANA YA KUWAFICHA WATOTO WALEMAVU MAJUMBANI MKOANI MBEYA

Kamanga na Matukio | 01:26 | 0 comments
Na Esther Macha, Chunya 
SERIKALI Wilayani Chunya Mkoani Mbeya imewataka watumishi wa serikali kuacha kujihusisha na masuala ya siasa kama watendaji  kwani wanachangia kuleta vurugu ndani ya wilaya badala yake wajikite kutatua kero za wananchi.
Kauli hiyo imetolewa jana  na Mkuu wa Wilaya ya Chunya ,Bw.Deodatusi Kinawiro wakati akitoa taarifa ya serikali katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri uliopo Wilayani humo.

Bw.Kinawiro alisema  kuwa  kazi kubwa ambayo wanatakiwa kuifanya watumishi wa serikali ni kuangalia hali ya usalama ndani ya wilaya na kutatua kero za wananchi ambazo zinawakabili ,suala la siasa lina wenyewe halipaswi kuwaingilia wahusika.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa kumeibuka tatizo kubwa kwa baadhi ya watumishi wa serikali kujihusisha na masuala ya siasa badala ya kazi za wananchi jambo ambalo si zuri kwani watumishi  badala ya kufanya kazi wanazotakiwa wamekuwa wakiacha na kubezi na siasa zaidi jambo ambalo si zuri.

Akizungumzia suala la usalama Bw. Kinawiro alisema kuwa kwasasa wilaya imekuwa shwari  hivyo  ni vema kuendelea kuhamasisha  ulinzi na usalama  ndani ya wilaya hii. “Ni juzi tu kumetokea vurugu za uchaguzi wa kijiji lakini wahusika walikamatwa na mpaka sasa wapo ndani ,kwani wilaya ya chunya haina tabia ya kuwa na vurugu”alisema Mkuu huyo wa wilaya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Bw.Chakupewa Makelele amesema  kuwa  suala hilo amelipokea atalifanyia kazi kwa kukaa na watumishi  wote wa halmashauri.

WALIMU WANAOJIHUSISHA KIMAPENZI NA WANAFUNZI KUFIKISHWA KATIKA VYOMBO VYA SHERIA.

Kamanga na Matukio | 01:25 | 0 comments
SERIKALI wilayani Mbarali Mkoani Mbeya imesema itawafikisha katika vyombo vya sheria walimu wote wanaojihusisha kimapenzi na wanafunzi, huku baadhi yao wakiwapa mimba na kuwageuza wake zao watoto hao wa shule.

Amesema  kuwa tabia hiyo ni uvunjaji wa maadili, na tabia ya kujihusisha kimapenzi na wanafunzi ni moja ya ubakaji kwa kuwa umri wa wanafunzi hao upo chini ya uangalizi wa walezi au wazazi.

Kauli hiyo imetolewa juzi na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Bw. Hussein Kiffu   wakati wa mkutano wa wadau wa elimu uliofanyika wilayani hapa katika ukumbi wa Rutheran .

Aliwataka walimu wenye tabia hiyo kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani ataanza kupita katika maeneo ili kupata taarifa za wanaume wanao/waliowapa mimba wanafunzi, huku viongozi wa eneo ambao hawakuchukua hatua zozote juu ya tatizo la mimba nao kusika kisheria.

 Aidha alisema kwa kuwa walimu ni walezi wa wanafunzi,  hawatakiwi kufanya suala lolote lililo baya kwa watoto hao,  nakwa mujibu wa sheria za nchi walimu watakaokutwa na makosa ya aina hiyo ya ubakaji watafungwa miaka isiyo chini ya miaka 30.

 “Walimu wanatakiwa kuwalea vyema watoto wetu, na ili kutokomeza tatizo hilo tumeanza kwa  kila mkuu wa idara anakuwa ni mlezi wa Kata, ili kuwaelekeza wananchi juu ya wajibu wao, na watakuwa chachu ya maendeleo katika ngazi ya kata, na kwa utawala tulionao tuache kufanya kazi kwa mazoea,” Alisema Kifu.

 Akitoa taarifa ya uchunguzi katika sekta ya elimu Wilayani humo, katibu mtendaji wa asas ya kiraia ya Usangu Non Governmental Organization Network (USANGONET) Bw.Paulo Kitha alisema mmomonyoko wa maadili wa wazazi, walimu na wanafunzi ni moja ya changamoto inayokwamisha sekta ya elimu wilayani humo, huku baadhi ya walimu kutokuwa na moyo wa kujituma katika kufanya kazi yao.

Bw. Kitha alisema baadhi ya walimu wamebainika kutokuwa na uwezo wa kutosha kufundisha huku mahusiano hafifu baina ya walimu na wazazi yakitoa fulsa kwa wanafunzi kuvunja maadili ya kitanzania.

Naye mratibu wa elimu Wilaya ya Mbarali Bw.Richard Kantamba akisoma taarifa ya ya elimu, alisema kuna uwepo wa wanafunzi zaidi ya elfu 11 wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Bw.Mantamba alisema tatizo hilo linatokana na uwepo wa changamoto mbalimbali ikiwemo yaupungufu mkubwa wa walimu, uhaba wa majengo ya shule, vyumba vya madarasa, nyumba za walimu pamoja na samani.

Aidha mratibu huyo alisema hata utoro uliokithiri kwa wanafunzi  ni sababu ya kiwango hicho cha wanafunzi kutojua kusoma, kuandika na kuhesabu, na kupelekea wilaya kutofanya vizuri katika matokeo ya mtiani wa darasa la saba.

Akitoa takwimu ya ufauru,Bw. Mtambe alisema Wilaya imekuwa ikisdhika nafasi ya mwisho katika matokeo hayo ambapo mwaka 2010 wilaya ilishika nafasi ya mwisho kimkoa, na mwaka 2011 kushika nafasi ya tano kati ya wilaya 8 za mkoa wa Mbeya.

 Mchungaji Jackob Mwabeya alisema changamoto nyingine ni pamoja na baadhi ya walimu kujihusisha kimapenzi na wanafunzi, huku badhi ya maofisa wakiwafanyia unyama walimu wanaokataa kuhusiana nao kimapenzi.

 “Hili tatizo linatupa hasara kubwa sisi wazazi, hapa kuna matatizo mengi, kuna baadhi ya maofisa elimu wamekuwa wakiwataka kimapenzi walimu wanaotoka vyuo na baada ya kukataa viongozi hao huwahamisha na kuwapeleka shule zenye changamoto kubnwa, kwa hiyo mwalimu anakuwa hana raha, anafanya kazi kwa hofu na mashaka,” Alisema Mwabeya.

Aidha Bw.Mwabeya aliongeza kuwa tabia ya kuna walimu ambao wamekuwa wakifanya ngono na wanafunzi jambo linalovchangia kutokuwepo kwa umakini kwa wanafunzi hao madarasani, huku wengi wao wakiwapa mimba pasipo kuchukuliwa hatua za kisheria.

Bw.Wiliard Sengele mkuu wa shule ya msingi Kapunga, alisema hata idadi kubwa ya wanafunzi katika vyumba vya madarasa ni sababu mojawapo inayochangia wanafunzi kutokuwa wasikivu darasani na hawathaminiwi kwani darasa moja linakuwa na zaidi ya wanafunzi 90

Bw.Brown Mwakibete alisema mabadiliko ya mitaala pasipo kuwapa mafunzo yoyote walimu dhidi ya mabadiliko hayo ni chanzo cha wanafunzi kutoelewa, na kuitaka serikali kutofanya mabadiliko pasipo kuwahusisha walimu.

Naye Bw.Abbubakari Chomba alisema baadhi ya watumishi sekta ya elimu ni mzigo kwani hawafahamu wajibu wao, huku wengine wakidiliki kuwa na matumizi mabaya ya fedha za mfuko wa maendeleo ya elimu (Capitation) kwa kujenga majengo chini ya kiwango, kwa kujali maslahi yao binafsi.

Mbunge wa jimbo la Mbarali Bw. Modestus Kilufi aliwataka watumishi kufuata maadili yao ya kazi, huku wazazi akiwataka kuwajibika ipasavyo kwa watoto wao ikiwa pamoja na kuwa na ushirikiano baina yao na walimu ili kwa pamoja kufanikisha malezi ya mwanafunzi.

Bw.Kilufi alisema moyo wa kujituma na uzalendo wa kweli wa kulipenda taifa ni nguzo muhimu katika kuinua sekta ya elimu kwa kuwawezesha wanafunzi kuyafikia malengo waliyojiwekea pasipo kuwakwamisha watoto wa kike kwa kuwapa mimba.

CCM MBARALI YACHARUKIA VIONGOZI WASIOWAJIBIKA.

Kamanga na Matukio | 02:16 | 0 comments
Mwnyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Bwana Mathayo Lauren Mwangomo, amesema kuwa wakati wakubezwa kwa chama hicho kwa sasa haupo  kutokana na kujisogeza kwa wananchi ili kupata changamoto zao.

 Ameyasema hayo katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Desemba 17 mwaka huu katika Kijiji cha Ruiwa wilayani humo.

Bwana Mwangomo amesema kuwa CCM imefanya mambo mazuri katika jamii ikiwa ni pamoja na kujenga shule za msingi na sekondari za kata, ambazo zimekuza kiwango cha elimu nchini ikiwa wapinzani wamekuwa wakibeza mafanikio hayo.

Pia amewataka wananchi kutokubali maneno ya uchochezi ambayo yamekuwa yakidhoofisha maendeleo  na juhudi za serikali  katika kutatua matatizo mbalimbali  na kwamba katika kuleta kasi hapakosi matatizo.

Katika Mkutano huyo Mwenyekiti huyo alipokea kero za wananchi wa kata ya Ruiwa ikiwa ni pamoja na ubadhilifu wa fedha zaidi ya shilingi milioni 60 zilizochangwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari ya Gwili ambazo zinadaiwa kufunjwa na Diwani wa kata hiyo Bwana Alex Mdimilage ambapo alimtorosha mhasibu  wa shule hiyo  na kutoroka na fedha za wananchi zaidi ya milioni 27 na kuiacha shule hiyo ikiwa haina chochote.

Kwa upande mwingine pia wamedai kuwa diwani huyo amekuwa kikwazo cha maendeleo ya kata hiyo na kutokana na uwajibikaji wake mbovu umepelekea wananchi wengi kukihama chama hicho.

Hata hivyo Diwani Mdimilage amekanusha tuhuma hizo na kudai kuwa mambo yote yanayozungumzwa dhidi yake ni chuki  za kisiasa na kwamba kwa kipindi chake hiki amesimamia miradi mbalimbali kijijini hapo na kata kwa ujumla.

Bwana Mwangomo amekiri kuwepo kwa viongozi wazembe katika  maeneo wilayani humo, hivyo amewataka viongozi wanaohusika  na tuhuma hizo kujiengua  mapema na hawatasubiri TAKUKURU na Polisi na kero zote zilizowasilishwa na wananchi atazifanyia kazi.

Katika ziara hiyo Mwenyekiti wa wilaya aliongozana na Geofrey Mwangulu  Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa, Patrick Mwaisomba(Mchumi wa Wilaya), Frank Mwashikumbulu ambaye ni mjumbe wa Halmashauri ya wilaya.


KADA WA CHADEMA AUAWA NYUMBANI KWAKE.

Kamanga na Matukio | 01:51 | 0 comments
Kada wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mtaa wa Sogea, Makambini mji mdogo wa Tunduma, Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya ameuawa na mtu au watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jumapili ya Desemba 16 mwaka huu nyumbani kwake.

Uchunguzi wa awali unadai kuwa kuma mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Meneck Kisunga, alienda nyumbani kwa marehemu, ambaye ni balozi wa mtaa huo akidai nyumbani kwake kuna ugomvi na mkewe hivyo kumtaka marehemu kwenda kusuluhisha ndipo marehemu alipofungua mlango alishambuliwa mpaka kuuawa.

Aidha Afisa  Mtendaji wa mtaa huo Bwana Osea Kabula amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na baadae alimtaarifu Mwenyekiti wa Mtaa huo Bwana Ally Mwafongo na hatimae kutoa taarifa kwa Jeshi la polisi Tunduma ambao walifika eneo la tukio kwa uchunguzi zaidi.

Mpaka sasa hakuna mtu yeyote aliyekamatwa kuhusiana na tukio hili na mazishi yamefanyika Desemba 17 mwaka huu katika makaburi ya Tunduma.

MLINZI AUAWA KIKATILI WILAYANI MBOZI MKOANI MBEYA

Kamanga na Matukio | 01:37 | 0 comments
Na Ezekiel Kamanga, Mbozi.
 Simon Mwambene(45) Mkazi wa Kijiji cha Matula, Mbozi Mission Kata ya Magamba Wilaya ya Mbozi, Mkoani Mbeya, ameuawa na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi alipokuwa lindo.

Marehemu ambaye alikuwa ni mlinzi wa binafsi na alikuwa analiza maduka 9 yaliyopo kijijini hapo na aliuawa na watu hao Desemba 13 mwaka huu majira ya saa 8:15 usiku.

Maduka hayo yaliyokuwa yakilindwa na marehemu yalikuwa yanamilikiwa na Bwqana Frank Tenson, Mgala, Tweve, Sosten Kibona, Raphael Kisunga, Kamika Simbeye, Crispin Ndabila, Gody Mahenge, Anthon Mwazembe na Samwel Ndabila.

Marehemu Mwambene alianza kulinda maduka hayo kwa mkataba kuanzia Desemba 3 mwaka 2011 ambapo hadi mauti yanmkuta alikuwa amefanya kazi kwa miezi 22, lakini kabla ya mauti hayo marehemu inadaiwa kuwa Desemba 12 mwaka huu majira ya saa mbili usiku alikuwa na ugomvi baina yake na mkazi mmoja Bwana Ezekia Sindwani. Ugomvi huo ulidumu kwa dakika sita na bwana Sindwani kudai hadharani kuwa atamfanyizia marehemu.

Aidha Bwana Sindwani akiwa na wenzake wanne Desemba 13 mwaka huu, majira ya saa 8:15 usiku walimvamia marehemu  wakiwa na vitu vyenye ncha kali walimpiga hadi kusababisha kifo chake papo hapo.

Baada ya kutenda tukio hilo la kikatili walivunja maduka hayo na kuiba mablanketi matano yenye thamani ya shilingi 37,500, vocha mia moja zenye thamani ya shilingi 100,000, mashuka matatu yenye thamani ya shilingi 20,000, Bia tatu za shilingi 6,000 vyote hivyo vikiwa na thamani ya shilingi 243,500.

Hata hivyo katika uchunguzi wa awali unaonesha kuwa Bwana Sindwani ni mzoefu katika vitendo vya kihalifu kama vile mwaka 2011 alituhumiwa kumuua Richard Nyemba, na mwaka 2000 alimuua Emmanuel Msongole.

Mpaka sasa Polisi Mkoani Mbeya wamefanikiwa kumtia nguvuni mshukiwa huyo na watu wanne wametoroka kusikojulikana.

BREAKING NEWS:- WATU WATATU WAGONGWA NA GARI MKOANI MBEYA MUDA HUU ......

Kamanga na Matukio | 12:31 | 0 comments

 Ajali mbaya imetokea eneo la ILEMI Jijini MBEYA muda huu ambapo gari aina ya TOYOTA LANDCRUISER iliokuwa ikitokea Wilaya ya Chunya imegonga watu watatu huyu ni mmoja wa waliogongwa. 

SAMAHANI KWA PICHA HII CHINI NIMELAZIMIKA KUIWEKA ILI UPATE HALI HALISI YA KILICHOTOKEA.
 Mwenyezi Mungu ambariki ili aweze kupona.
Gari aina ya TOYOTA LANDCRUISER iliokuwa ikitokea Wilaya ya Chunya imegonga watu watatu huyu ni mmoja wa waliogongwa.

BREAKING NEWS:- MTOTO AUMWA NA NYUKI HADI KUPOTEZA MAISHA.

Kamanga na Matukio | 02:46 | 0 comments
Mtoto wa miaka mitatu na nusu Abiud Moses Mwanyingili mkazi  wa kijiji cha Mponela wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya amefariki dunia baada ya kung'atwa na nyuki alipokuwa akicheza na wenzie kijijini hapo Desemba 13 mwaka huu majira ya saa nane mchana.

Katika tukio hilo kundi la nyuki halikuweza kufahamika limetokea wapi, mbali ya kusabaisha kifo hicho pia nyuki hao wamesababisha kifo kwa Ester Kasebele miaka 6 ambaye amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi mkoani hapa.

Aidha Mwenyekiti wa kijiji cha Mponela Bwana Laniwelo Mwampashi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mazishi ya mtoto huyo yamefanyika kijijini hapo baada ya kufanyiwa uchunguzi na Daktari wa hospitali ya wilaya hiyo.

Wakati huohuo mlinzi aliyefahamika kwa jina moja la Mwanzembe ameuawa kikatili na mtu au watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, karibu na lango la hospitali ya wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi mkoani hapa Diwani Athumani amwthibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba jeshi lake linafanya uchunguzi kuhusiana na tukio hilo na taarifa zaidi zitatolewa na hakuna mtu yeyote aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYAHABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 14/12/2012.

Kamanga na Matukio | 02:33 | 0 comments



WILAYA YA CHUNYA - TAARIFA KUOKOTWA KWA SILAHA [BASTOLA].
MNAMO TAREHE 12.12.2012 MAJIRA YA SAA 09:00HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA IFUMBO WILAYA YA CHUNYA MKOA WA MBEYA. WATOTO WADOGO WALIOKUWA WAKICHEZA MPIRA WA MIGUU KATIKA UWANJA WA S/MSINGI IFUMBO WALIOKOTA BASTOLA MOJA ILIYOTENGENEZWA KIENYEJI INAYOTUMIA RISASI ZA S/GUN IKIWA NA RISASI MOJA YA S/GUN . MBINU NI KUHIFADHI SILAHA HIYO KATIKA MFUKO WA RAMBO NA KUIWEKA KANDO YA UWANJA HUO . KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUTOMILIKI SILAHA BILA YA KIBALI KWANI NI KOSA LA JINAI. AIDHA ANATOA RAI KWA WAZAZI/WALEZI KUWAELIMISHA WATOTO KUACHA TABIA YA KUOKOTA NA KUCHEZEA VITU AMBAVYO HAWAVIFAHAMU KWANI VINGINE VINAWEZA KUWA  NI VITU VYA HATARI/MILIPUKO NA BADALA YAKE WATOE TAARIFA KWA WAZAZI/WALEZI AU MAMLAKA HUSIKA ILI HATUA ZA HARAKA ZICHUKULIWE KUEPUSHA MADHARA YANAYOWEZA KUJITOKEZA.KAMANDA PIA ANARUDIA KUTOA WITO KUWA KIPINDI HIKI NI CHA ‘”OFFER “ YA KUSALIMISHA SILAHA BILA KUCHUKULIWA HATUA NA KINAMALIZIKA TAREHE 05.01.2013. ANATAHADHARISHA USALIMISHAJI UYALENGE MAENEO YALIYOSALAMA ZAIDI TOFAUTI NA ILIVYO KUWA KWA SILAHA HII KWA KUWA SILAHA INAWEZA KUANGUKIA KWA WATU WASIOWEMA.

WILAYA YA CHUNYA - TAARIFA YA KUPATIKANA KWA RISASI ZA SMG
MNAMO TAREHE 12.12.2012 MAJIRA YA SAA 15:00HRS HUKO KATIKA HIFADHI YA LUKWATI ILIYOPO KATIKA KIJIJI CHA BITIMANYANGA WILAYA YA CHUNYA MKOA WA MBEYA . DAIMON S/O JOHN, MIAKA 32, MNYAMWEZI, ASKARI MGAMBO MKAZI WA BITIMANYAGA AKIWA KWENYE DORIA YA KUDHIBITI MAJANGIRI KATIKA PORI HILO NA ASKARI MGAMBO WENZAKE WAWILI WALIMUONA MTU MMOJA ASIYEFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE JINSIA MWANAUME AMBAYE ALIWAKIMBIA NA KUTOKOMEA PORINI BAADA YA KUTUPA KIFURUSHI KIMOJA AMBACHO NDANI YAKE KULIKUTWA RISASI 114 ZA SMG, NGUO NA REDIO MOJA NDOGO AINA YA AITKENSON AMBAYO JUU IMEANDIKWA JINA LA MBOGE. MBINU NI KUKIMBIA NA KUTELEKEZA KIFURUSHI HICHO BAADA YA KUWAONA ASKARI MGAMBO HAO. MTUHUMIWA ANADHANIWA KUWA NI MUWINDAJI HARAMU.KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUTOMILIKI SILAHA BILA YA KIBALI KWANI NI KOSA LA JINAI.AIDHA ANATOA RAI KWA MTU/WATU WENYE TAARIFA JUU YA ALIKOJIFICHA MTUHUMIWA HUYO AZITOE KWA MAMLAKA HUSIKA ILI AKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.

Signed By,
[  DIWANI ATHUMANI – ACP  ]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

HABARI KAMILI KUHUSU UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA SONGWE MBEYA WAANZA KUTUMIKA NDEGE ZAIDI YA TATU ZATUA

Kamanga na Matukio | 02:31 | 0 comments

Mwandishi wa habari kutoka Kituo cha redio kinachofahamika kutoka Nyanda za Juu Kusini Bomba FM na Blogu ya Kamanga na Matukio Ndg. Ezekiel Kamanga akishuka katika ndege katika uzinduzi wa uwanja huo wa Ndege wa kimataifa uliopo Songwe Mkoani Mbeya. 
Brandy Nelson,Mbeya
HATIMAYE  Ndege ya  kwanza ya abiria  imetua  katika Uwanja wa kimataifa wa Songwe rasmi leo baada ya miaka 11 ujenzi wake ambao  tayari umekamilika na kugharimu kiasi cha sh.100 bilioni.

Akizungumza  baada ya kutua ndege hiyo  Kaimu Mkurugenzi wa malamalaka ya Viwanja vya ndege Tanzania (TAA) Seleman  Seleman alisema kuwa tayari uwanja wa kimataifa wa Songwe umekamilika na dunia nzima inataarifa ya  kukamilika kwa uwanja huo.

Alisema kuwa kutokana na kukamilika kwa uwanja huo tayari ofisi za mamalaka hiyo imeshahamia katika uwanja huo na kuanza shughuli zake rasmi leo ambapo uwanja wa zamani  umefungwa rasmi hakuna ndege yoyote itakayoweza kutua katika uwanja huo.

“Kimeanzisha historia mpya kwani dunia inafahamau kwa asasa kwamba uwanja wa kimataiafa wa Songwe upo wazi umekamilika na umeanza kutumika rasmi leo”alisema

Alisema kuwa Uwanja wa songwe wa kimataifa ni  kati ya  viwanja vikubwa viwili  kujengwa  baada ya uhuru ukitanguliwa na uwanja wa  mkoa wa Kilimanjaro kwani viwanja vingine vimekuwa vikifanyiwa marekebisho.

Kwa upande wake kaimu mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Mkuu wa Wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro alisema aliwataka wananachi wa Mkoa wa Mbeya kujiandaa kutumia uwanja huo kwa kuongeza kipato chao na kuinua uchumi wa Mkoa.

Alisema kuwa Wakazi wa Mbeya wanaopaswa kuzalisha kwa wingi maua na matunda ili kutumia vizuri uwanja huo ili uchumi wa mkoa uweze kukua “tusiutumie uwanja huu kwa lengo la kusafiria pekee”alisema

“Uwanja wa Songwe ni fulsa muhimu  kwa wakazi wa mkoa wa Mbeya na mikoa jirani kwani utaweza kuwasaidia katika kuongeza pato la mtu mmoja mmoja na taiafa kwa ujumla kutokana na uwanja huo kuwa wa kimataifa ambapo shughuli mbali mbali za  kiuchumi zitafanyika kutokana na uwanja huo”alisema

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger