Pages


Home » » WANAWAKE WATAKIWA KUJIHUSISHA NA UJASIRIAMALI

WANAWAKE WATAKIWA KUJIHUSISHA NA UJASIRIAMALI

Chimbuko Letu | 10:16 | 0 comments
Na Ezekiel Kamanga,Chunya.

Wanawake wa halmashauri ya wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya wametakiwa kujihusisha na ujasirimali ili waweze kufikia malengo ya hamsini kwa hamsini na kuachana na dhana  ya kutegemea  wanaume pekee kama ndio wazalishaji wakuu katika familia.

Haya yameelezwa na mwenyekiti wa UWT wilaya ya Chunya Mboka Konzo wakati akizungumza na mwandishi wa habari kuhusiana na mwamko wa wanawake wa halmashauri ya Chunya kujihusisha na shughuli za ujasirimali ukilinganisha na miaka ya nyuma.

Konzo alisema mwamko wa wanawake kwa halmashauri ya Chunya kwasasa umekuwa mkubwa ukilinganisha  miaka ya nyuma  walikuwa wakitegemea wanaume kwa kila kitu huku wao wakibaki nyumbani waletewe chochote lakini kwasasa wanawake wanajishughulisha na  ujasirimali mdogo mdogo kama kuuza mboga mboga,mamamntilie na hata kuzungusha matunda.

Aliendelea kueleza kuwa mbali na kuwa na kasi ya kujihusisha na ujasiriamali wanawake wamekuwa wakiungana katika vikundi vya kukopa na kurejesha (upatu)ambavyo vimekuwa vikiwawezesha wanawake wengi kujikwamua kiuchumi.

Aidha wakizungumzia suala la ujasiliamali baadhi ya wajasirimali wadogo wadogo Esta George na Rehema Charles wanaojihusisha na uuzaji wa matunda katika stend ya chunya mjini walisema kuwa kwasasa wanajitambua na kwamba wameamua kujihusisha na ujasiriamali kama njia ya kusaidiana katika majukumu.

Ambapo waliongeza kuwa licha ya kusaidiana katika majukumu wanafanya hivyo ili kesho na kesho kutwa mwanaume asipokuwepo waweze kusimama wenyewe na kuendesha familia zao bila kuteteleza kwani wamekuwa wakiona wanawake wenzao ambao wamekuwa wakitegemea wanaume jinsi wanavyohangaika wanapoondokewa na waume zao.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger