Pages


Home » » UHAMIAJI HARAMU, UINGIZWAJI WA POMBE HARAMU NA DAWA ZA KULEVYA WAZIKUTANISHA WILAYA MBILI ZA TANZANIA NA MALAWI KUJADILI SULUHISHO.

UHAMIAJI HARAMU, UINGIZWAJI WA POMBE HARAMU NA DAWA ZA KULEVYA WAZIKUTANISHA WILAYA MBILI ZA TANZANIA NA MALAWI KUJADILI SULUHISHO.

Chimbuko Letu | 10:25 | 0 comments
 Mkuu wa Wilaya ya Kalonga, Nchini Malawi Rosemary Kalonga na Mkuu wa Wilaya ya Kyela Dk Thea Ntara.
 Maafisa Usalama kutoka Wilaya ya Kyela nchini Tanzania.
 Maafisa Usalama kutoka Wilaya ya Karonga nchini Malawi.
 Maafisa Mifugo kutoka Wilaya za Kyela na Karonga


Kikao cha ujirani mwema baina ya Wilaya ya Kyela nchini Tanzania na Karonga nchi ya Malawi kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela kwa ajili ya kujadili changamoto zinazozikabili Wilaya hizo.
Wilaya ya Kyela iliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya Dakta Thea Ntara na kwa upande wa Wilaya ya Karonga iliwakilishwa na Rosemary Moyo na baadhi ya changamoto kubwa zinazozikabili Wilaya hizo ni pamoja na wahamiaji haramu,madawa ya kulevya,pombe kali na wizi wa pikipiki.
Baadhi ya wajumbe kutoka pande zote mbili wamesema kuwa tatizo la wahamiaji haramu kutoka nchi za Ethiopia,Somalia,Congo,Burundi,Rwanda na Nigeria kunachangiwa na ukoefu wa umakini kutoka mipaka ya kaskazini ambapo huwaacha wahamiaji hao kuingia kiholela.
Sababu nyingine inachangiwa na baadhi ya watumishi wa umma wa pande hizo mbili  wa kutodhibiti vitendo hivyo kutokana wa baadhi ya wahamiaji kutumia pesa pindi wanapokamatwa na baadhi ya maafisa usalama wasio waaminifu.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Karonga Rosemary Moyo amesema kuwa Watanzania na Wamalawi ni ndugu wa damu ambao wametenganishwa na wakoloni kwa njia ya mpaka wa mto Songwe kwani mpaka sasa raia wa mpakani huvuka kutembeleana kila siku na wengi wao wameoleana kutoka pande hizo mbili.
Hata hivyo kutokana na tatizo hilo kubwa kwa nchi hizo Serkali zote huingia gharama kubwa kuwatunza na kuwasafirisha wahamiaji haramu  kuwarejesha nchi walizotoka.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kyela Dakta Thea Ntara amesema wilaya ya Kyela imeimarisha ulinzi mpakani kwa kushirikiana na wananchi ndiyo maana wamefanikiwa kukamata wahamiaji wengi haramu waliojaribu kuvuka mpaka kupitia wilaya hiyo hivyo juhudi kubwa zifanyike ili kuhakikisha tatizo hilo linakomeshwa kabisa.
Hata hivyo elimu itolewe kwa raia wa pande zote mbili ili watu wanaowatilia shaka watolewe taarifa katika vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hizo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger