Pages


Home » » Mwenyekiti ashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya kwa tuhuma kufuja mali.

Mwenyekiti ashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya kwa tuhuma kufuja mali.

Chimbuko Letu | 08:47 | 0 comments
Na Ezekiel Kamanga.
Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linawashikilia Mwenyekiti wa Kitongoji cha Nsalala Stephano Mshani(CHADEMA)na Mtendaji Lwitiko Mwaibindi kwa tuhuma za kuuza ardhi ya Kijiji na fedha kujimilikisha kwenye akaunti mbili za Mwenyekiti.

Tukio hilo limetokea katika mkutano wa hadhara baada ya wananchi kuwatuhumu viongozi hao kwa kuuza mali ya umma kisha kujimilikisha jumla ya shilingi milioni nane laki sita na elfu hamsini bila ridhaa ya wananchi wa kitongoji cha Nsalala.

Katika mkutano iliofanyika machi 26 mwaka huu wananchi hao walimwandikia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Upendo Atu Sanga wakitaka kuundwa kwa Tume ya uchunguzi ili kubaini fedha zinazodaiwa kuhodhiwa na viongozi hao bila ridhaa ya wananchi.

Baada ya kupokea malalamiko hayo Mkurugenzi alituma Tume ya uchunguzi ambapo ilibaini tuhuma mbalimbali dhidi ya viongozi hao na kuyasoma maagizo mbele ya mkutano wa hadhara uliofanyika April mosi mwaka huu katika uwanja wa shule ya msingi Nsalala.

Barua hiyo kutoka kwa Mkurugenzi ilisomwa mbele ya wananchi na Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Prosper Msivala amabayo ilibaini kuwa :-

(a)Mwenyekiti Stephano Mshani anatuhumiwa kwa makosa yafuatayo:-
(i)Kushiriki kuuza mali ya Umma kinyume cha sheria ya manunuzi ya Umma ya mwaka 2011.
(ii)Kutunza fedha zilizotokana na mauzo hayo kwenye akaunti zake binafsi mbili zilizopo Benki ya NMB Mbalizi Road zenya namba 6251000804 na 62510009 zote zikimilikiwa na Stephano Mshani.

(b)Mtendaji wa Kitongoji(Lwitiko Mwaibindi)anatuhumiwa kwa:-
(i)Matumizi mabaya ya madaraka kwa kushindwa kusimamia Kitongoji na kuwapotosha wananchi.
(ii)Kughushi nyaraka na mikhutasari ya vikao
(iii)Kukodisha eneo la maziko kwa shughuli za kilimo bila kufuata taratibu.
(iv)Kuuza mali ya Umma kinyume na taratibu ya manunuzi ya Umma ya mwaka 2011.
(v)Matumizi mabaya ya muhuri ambao siyo halali.
(vi)Kumdanganya Mwajiri kwa kuficha ardhi ya Mamlaka na kutokabidhi kwa mamlaka.

Hivyo kutokana na makosa hayo Mkurugennzi Mtendaji wa Wilaya ameagiza mosi eneo lililouzwa kurudishwa mara moja kwenye Maml;aka ya Mji mdogo kuanzia April mosi mwaka huu.

Pili Mtendaji wa Kitongoji(Lwitiko Mwaibindi)anasimamishwa kazi kuanzia April mosi mwaka huu ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili.

Tatu Polisi na vyombo vya Dola vimchukulie hatua stahiki Mwenyekiti wa Kitongoji cha Nsalala Stephano Mshani.

Uchunguzi umebaini kabla ya mkutano huo viongozi hao walikuwa na taarifa mbili za mapato na matumizi yenye kuonesha kuwa baadhi ya wadau walichanga jumla ya shilingi milioni tatu laki nane arobaini na tatu elfu(3,843,000/=) ambazo zilitumika zote kununua vifaa vya ujenzi,malipo ya mafundi na kusafirishia vifaa vya ujenzi kwa ajili ya shule ya msingi Nsalala.

Taarifa ya mauzo ya shamba shilingi 8,650,000/= ambazo zinaonesha kununulia vifaa vya ujenzi fedha ambazo zilitunzwa kwenye akaunti binafsi za Stephano Mshani kuwa akaunti ya Kitongoji ilikuwa haifanyi kazi kwa muda mrefu.

Baada ya Mwanasheria kuisoma barua hiyo kutoka kwa Mkurugenzi Stephano Mshani na Lwitiko Mwaibindi walichukuliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano na Diwani wa Kata ya Nsalala Kissman Ngomale alifunga mkutano kwa kuwataka wananchi kuwa wavumilivu ili kusubiri hatua stahiki dhidi ya viongozi hao ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger