Pages


Momba, wamependekeza Mkoa mpya utakaogawanywa na serikali upewe jina la Momba, ukijumuhisha Wilaya ya Momba, Mbozi, Ileje na Chunya huku makao makuu yakiwa Vwawa.

Kamanga na Matukio | 03:57 | 0 comments

 Mkuu wa Wilaya ya Momba, Abiudi Saideya amesema Mkoa wa Mbeya utabaki kama ulivyo huku ukiunganisha Wilaya ya Mbeya, Kyela, Rungwe na Mbarali.
Mkurugenzi Halmashauri ya Momba
Wakitoa mapendekezo yao baadhi ya wajumbe, walisema kuwa Wilaya ya Momba inavivutio vya kiutalii, idadi ya watu, mazao ya chakula na biashara kama vile ufuta, kahawa, mahindi, mpunga  pamoja na uoto wa asili.


Timu ya wataalamu wa halmashauri ya Wilaya ya Momba, wamependekeza Mkoa mpya utakaogawanywa  na serikali upewe jina la Momba, ukijumuhisha Wilaya ya Momba, Mbozi, Ileje na Chunya huku makao makuu yakiwa Vwawa.
Pendekezo hili wamelitoa jana, kwenye kikao cha Kamati ya ushauri kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo eneo la Ukwile Wilayani Mbozi kutokana n kutokamilika kwa baadhi ya miundombinu ya wilaya ya Momba.
Kikao hicho kilichokuwa kikijadili maendeleo ya Wilaya kiliendeshwa na Mkuu wa Wilaya ya Momba, Abiudi Saideya na kwamba Mkoa wa Mbeya utabaki kama ulivyo huku ukiunganisha Wilaya ya Mbeya, Kyela, Rungwe na Mbarali.
Aidha, mapendekezo hayo yamekuja ni baada ya Rais wa Jamuhuri ya Muunganano akiwa Mkoani Mbeya kwenye sherehe za mei mosi kuridhia ombi la serikali kuugawa Mkoa wa Mbeya kutokana na ukubwa wa eneo za mraba zilizopo.
Wakitoa mapendekezo yao baadhi ya wajumbe, walisema kuwa Wilaya ya Momba inavivutio vya kiutalii, idadi ya watu, mazao ya chakula na biashara kama vile ufuta, kahawa, mahindi, mpunga  pamoja na uoto wa asili.
“Momba ndio kitovu cha barabara kuu iendayo nchi za kusini mwa Afrika endapo utapewa hadhi ya Mkoa utaongeza kipato kupitia ushuru wa forodha kwa nchi za kusini mwa afrika,”alisema Saideya
 Pia, kikao hicho kilitumia nafasi hiyo kutoa onyo kwa baadhi ya wananchi ambao wamekuwa wakijichukulia sheria mkononi na kusababisha vifo vya watu kutokana na vitendo vya kishirikina ambavyo vimetajwa kukithiri katika Wilaya hiyo.
Saideya, aliwataka waganga wa kienyeji ambao wanashughulika na upigaji wa ramli kuacha mara moja kwani wao ndio chanzo cha mauaji hayo.
Alisema, waganga wanapopiga ramli huwataja baadhi ya watu kwamba ndio wamesababisha kifo cha mgonjwa Fulani hivyo kupelekea watu kutengeneza uadui hadi kufika mahala wananchi kujichukulia sheria mkononi kwa kuondoa uhai wa watu hao wanaotajwa na waganga.

“Hivi karibuni katika kijiji cha Msangano, watu watatu walizikwa wakiwa hai kutokana na ramli hizi za waganga jambo linalotia dosari Wilaya ikiwa na kudumaza maendeleo kwani watu wanaogopa kuwekeza biashara zao,”alisema
Hata hivyo, Mkuu huyo aliwataka wakazi wa eneo hilo kujenga tabia ya kutunza chakula hasa kwenye msimu huu wa mavuno kwani kumekuwepo na dalili za nje kutokana na hali ya ukame inayoendelea Wilayani humo.

Picha na Ezekiel Kamanga

MEELA ASIKIKITISHWA NA HALI YA WANAHABARI MBEYA, ATIA MKONO KUANZISHA SACCOS

Kamanga na Matukio | 03:56 | 0 comments

MKUU wa wilaya ya Rungwe Bw. Chripin Meela amesema, changamoto zinazokabili sekta ya habari na  vyombo vya habari  kwa ujumla ni matokeo ya umuhimu wa taaluma hiyo katika ukuaji wa demokrasia nchini
Wana habari wa Mbeya wakimsikiliza mkuu wa Wilaya Rungwe



MKUU wa wilaya ya Rungwe Bw. Chripin Meela amesema, changamoto zinazokabili sekta ya habari na  vyombo vya habari  kwa ujumla ni matokeo ya umuhimu wa taaluma hiyo katika ukuaji wa demokrasia nchini.
Akizungumza kwenye mkutano wa uchaguzi wa klabu ya wandishi wa habari mkoa  Mbeya Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispin Meela amesema, wananchi wana matumaini makubwa na vyombo vya habari na pale kipapota doa la utendaji ni muhimu kujirekebisha kabla ya kutengeza picha mbaya mbele ya jamii wanayoihudumia.
Amesema hali iliyojitokeza hivi karibuni kwenye klabu hiyo inahitaji kuweka misingi imara ya kiutendaji  na kwamba jitihada za kufanya uchaguzi  wakati huu ni hatua muhimu za kuimarisha mfumo wa kujiwajibisha kama taasisi ya taaluma.
Amesema ikiwa viongozi wa dini na vyombo vya habari vitajihusisha na ubadhirifu na wizi ni dalili kuwa hakutakuwa na mwingine wa kukemea jamii itakayokuwa huru na yenye kukemea vita dhidi ya rushwa.
Bwana Meela amesema inashangaza kuona hata vyombo vya habari vinaingia kwenye ufisadi na akaohoji  ninani atakayehoji ufisadi serikali na kwingineko kama nanyi mnaingia kwenye mitego hiyo hiyo?.
Katika hatua nyingine amependekeza  Vyombo vya habari kujenga utamaduni wa kujihusisha na ufuatiliaji wa maendeleo vijijini na kwa kufanya hivyo kutawezesha wananchi kuwasilisha changamoto zinazowakabili kwa watunga sera.
Amesema katika kufikia hilo  ni vyema pia Viongozi wa serikali ngazi za chini kuondoa uoga  katika kufanya kazi na vyombo vya habrari na kwa kufanya hivyo kutasadia kusukuma mbele jitihada za maendeleo.
Katika hatua nyingine Bwana Meela amechangia kiasi cha shilingi 400,000 kwaajili ya uanzishaji wa chama cha kuweka na kukopa cha wanahabari  SACCOS  ili kuwezesha kuwapa fulsa wana habari  kujisimamia kiuchumi  na kupunguza changamoto za kimaisha zinazowakabili.
Katika kufanikisha hilo wanachama wa Mbeya Press club walijitokeza kuchangishana wenyewe ambapo wamefanikiwa kukusanya mtaji wa papo kwa papo kiasi cha shilingi 1,400,000/=.
Aidha ameshauri klabu ya wandishi wa habari kuwa na ofisi yake na hvyo kwa kuomba kiwanja kwenye mamlaka za majiji itasaidia kuwapa nguvu katika kusimamia haki zao wakiwa na uhuru wa kuwekeza kwenye majengo yao.

Habari na Indaba Africa

picha na Mbeya yetu

SHULE ya msingi ya Idugumbi iliyopo Mbeya vijijini, inakabiliwa na uhaba wa wanafunzi kutokana na wazazi kuwatumia watoto hao kwenye shughuli za uvunaji wa zao la kahawa.

Kamanga na Matukio | 03:55 | 0 comments
SHULE ya msingi ya Idugumbi iliyopo Mbeya vijijini, 
Mwalimu Mkuu wa shule ya Idugumbi Mpaze Mchaba, amesema licha ya shule hiyo kuwa na madarasa ya kutosha , madawati pamoja na walimu lakini watoto waliopo ni 270.
Akizungumzia tatizo hilo Mtendaji wa kijiji cha Idugumbi Deodath Msyaliha, amekiri kuwepo kwa utoro wa wanafunzi pamoja na wazazi kuwatumia watoto kwenye shughuli hizo za uzalishaji kwa kutumia kilimo cha kahawa.
Wanafunzi wachache waliofika shuleni
Baadhi ya wazazi walioitwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo wakimsikiliza mwalimu huyu juu ya watoto wao kutofika shule
“Baada ya kubaini tatizo hili tulilifikisha kwenye serikali ya kijiji na kuazimia kuwa kila mtoto atakaye toroka shule mzazi atawajibika kutoa shilingi 2000 kila siku atakaye kosa masomo tukiamini wazazi watajirekebisha na kuwahimiza watoto kufika shuleni  hali ambayo ni tofauti,”alisema



Shule ya msingi ya Idugumbi iliyopo Mbeya vijijini, inakabiliwa na uhaba wa wanafunzi kutokana na wazazi kuwatumia watoto hao kwenye shughuli za uvunaji wa zao la kahawa.
Akizungumzia tatizo hilo, Mwalimu Mkuu wa shule ya Idugumbi Mpaze Mchaba, alisema licha ya shule hiyo kuwa na madarasa ya kutosha , madawati pamoja na walimu lakini watoto waliopo ni 270.
Alisema, uhitaji wa shule ni watoto zaidi ya 400 lakini mpaka sasa ni watoto 270 ndio wanaohudhuria masomo darasani na kati yao ni watoro wa kudumu.
Alisema, kamati ya shule ilifanya uchunguzi na kubaini kuwa baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwatumikisha watoto kwenye shughuli ya kilimo kama vile kuvuna kahawa na kupeleka viwandani.
“Baada ya kubaini tatizo hili tulilifikisha kwenye serikali ya kijiji na kuazimia kuwa kila mtoto atakaye toroka shule mzazi atawajibika kutoa shilingi 2000 kila siku atakaye kosa masomo tukiamini wazazi watajirekebisha na kuwahimiza watoto kufika shuleni  hali ambayo ni tofauti,”alisema.
Akizungumzia tatizo hilo Mtendaji wa kijiji cha Idugumbi Deodath Msyaliha, amekiri kuwepo kwa utoro wa wanafunzi pamoja na wazazi kuwatumia watoto kwenye shughuli hizo za uzalishaji kwa kutumia kilimo cha kahawa.
Aliwataja baadhi ya wazazi hao kuwa ni Isaya Waziri, Yohana Waziri, Julius waziri na Msuya Waziri ambao wote kwa pamoja walikiri kwa maandishi mbele ya kamati ya shule kuhusika na ukatishaji watoto masomo na kukubali kulipa lakini mpaka sasa hawajatekeleza.
Aidha, Mtendaji huyo, alisema suala hilo limefikishwa kwenye ofisi ya Mtendaji Kata na Diwani ili watuhumiwa hao washughulikiwe kwa kuwakatisha watoto masomo darasani kama taratibu za elimu zinavyoeleza.
Wakati huo huo, Shule ya msingi ya Mbalizi na Mageuzi zinatarajiwa kufunguliwa hivi karibuni baada ya kufungwa kwa zaidi ya miezi miwili kutokana na ukosefu wa matundu ya vyoo.
Akizungumzia hilo Mwenyekiti wa kijiji cha Mapinduzi Nelsoni Mwakyusa, alisema kijiji kilitoa shilingi 200,000 katika kukamilisha ujenzi wa matundu  24 ya vyoo vipya ambapo matundu ya awali yalititia kutokana na mvua za masika.
Alisema, kutokana na tatizo hilo shule hizo hazitakuwa na likizo katika kufidia muda ambao watoto walikaa nyumbani na kukosa masomo kwa zaidi ya miezi miwili.
Picha na Ezekiel . Kamanga

Wazazi kukwepa majukumu katika familia zao ni chanzo cha watoto kujiajiri Mkoani Mbeya.

Kamanga na Matukio | 03:16 | 0 comments

KUSHOTO MTOTO COLYNS JOHN MIAKA 8 MWANAFUNZI WA DARASA LA PILI SHULE YA MSINGI IKUTI JIJINI MBEYA NA LUSHINDIHO SIMKONDA MIAKA 10 HUYU HASOMI KABISA SHULE HAPA WAMEAJIRIWA KUBEBA TOFARI KWA UJIRA WA SHILINGI 30 TU KWA TOFARI MOJA

HUYU NI ANNA  SAIMON MIAKA 8 NI MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI IKUTI DARASA LA TATU  AKIWA AMEBEBA TOFARI MBILI ZINAZOKADIRIWA KUWA NA UZITO WA KILO 10 


WATOTO HAWA TULIPOWAULIZA KWANINI MNABEBA TOFARI HIZI MUDA WA KUWA SHULE WALITUJIBU KUWA TUNATAFUTA HELA ZA DAFTARI KWANI WAZAZI WETU HAWANA UWEZO WA KUTUNUNULIA

WATOTO HAWA TULIWAFUATILIA AMBAPO WALITEMBEA KWA UMBALI WA MITA 500 KUZIFIKISHA TOFARI HIZO HUKU JUA KALI  LIKIWAWAKIA NA BILA YA KUWA NA VIATU MIGUUNI MAJIRA YA SAA 7 MCHANA WENZAO WAKIWA MADARASANI 


MTOTO COLYNS JOHN MIAKA 8 AKILIA BAADA YA KUELEMEWA NA UZITO WA TOFARI ALIZOBEBA KWANI AKIZIVUNJA TU HAWEZI LIPWA PESA YAKE JAMANI INAUMA SANA WAHUSIKA MPO WAPI? JUU YA SWALA HILI LA AJIRA KWA WATOTO



KUSHOTO NI FREDRICK SIMON MIAKA 12 AKIMSIHII COLNSY ASILIE KUWA SASA ANAKARIBIA KUFIKA



BINTI HUYU AMETOKA KUCHOTA MAJI MTO NZOVWE


Picha na Ezekiel Kamanga

UCHAFU WAKITHIRI SOKO LA IKUTI JIJINI MBEYA

Kamanga na Matukio | 03:15 | 0 comments







Wananchi wa Kata ya Iyunga mtaa wa IKuti  jijini mbeya wamelalamikia kitendo uongozi wa jiji la mbeya kushindwa kuzuia hali ya uchafu katika eneo la soko la Ikuti jijini

          Licha ya kuwepo kwa shughuli za kimaendeleo hasa soko na shughuli nyiingine hali imekuwa mbaya katika eneo la soko hilo kutokana na kuwepo kwa mirundikano ya uchafu katika ya soko hilo.

          Wakizungumza juu ya kuwepo kwa hali hiyo  wananchi wa maeneo hayo wamedai kuwa takataka zilizo jazana katika eneo hilo la soko linahatarisha afya za wakazi wa eneo hilo kutokana kuwepo na huduma muhimu kama soko ambako kunauzwa vyakula na mahitaji mengine.

        Mmoja wa wakazi hao ndugu  Janneth Mbukwa amesema kuwa kwa muda mrefu sasa takataka hizo zimekuwepo eneo hilo licha ya wafanyabiashara wa eneo hilo pamoja na baadhi ya wananchi kutoa taarifa sehemu husika ili kulifanyia kazi suala hilo.

        Amesema kuwa licha ya kuwepo kwa uchafu huo  kwa muda mrefu bado mawakala wa kutoza ushuru wamekuwa wakikusanya michango kama kawaida    Licha ya kuwepo kwa hali hiyo ambayo ni adha kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo.

        Amesema tatizo kubwa lililopo katika eneo hilo ni harufu mbaya inayo toka eneo hilo ambapo kwa asilimia kubwa huathiri shughuli  zilizopo katika eneo hilo ambapo zaidi ya vibanda 20 vya mama ntilie  vipo eneo hilo la ghuba la taka hali ambayo imefanya wateja wao kuwa na hofu juu  ya afya zao.

Mtoto wa miaka miwili afungiwa ndani zaidi ya miaka miwili Mkoani Mbeya.

Kamanga na Matukio | 02:16 | 0 comments

Mtoto Joshua akiwa amekaa uwani kwenye nyumba  yao huku wazazi wake wakiwa wamemwacha peke yake toka asubuhi bila ya kumpatia chakula mtoto huyo tumemkuta katika hali mbaya sana kwani tunemkuta amejisaidia haja ndogo na hana hata nguo za kubadilisha


Kwa ujumla mtoto Joshua hata kutembea hawezi kwani simama yake ni ya kutetemeka migu tu 

Hizi ni nguo za joshua na kaka yake nguo hizi hazifuliwi bali zikirowa na mkojo huwanikwa tu juani na kisha kuvaliwa tena

Mtoto Joshua akiwa ana tushangaa maana anaona amevamiwa kwakweli inasikitisha sana

Hapa ndiyo mtoto joshua huwa anacheza wakati wa mchana

Mlango ulio wazi ndimo mtoto Joshua hufungiwa humo

Hiki ndicho chumba mtoto Joshua hufungiwa kama picha unavyoiona kona hiyo ndiyo mtoto huyo hujibanza


Kushoto ni kaka wa Joshua yeye amesema huwa anashinda nyumba za jirani kucheza wakati mdogo wake amefungiwa ndani

Mama wa mlezi wa Joshua akiingia numbani kwake na kutushangaa tumekuja fuatanini kwake

Angalia picha hii kwa makini jinsi mtoto Joshua anavyomwangalia mama yake mlezi yaani mama wa kambo

Sekera Watsoni (40) amembeba mtoto Joshua kuonyesha anampenda na kuwa anamhudumia vizuri mtoto huyo

Huyu mama pamoja na mumewe ndiyo wanaomtesa mtoto Joshua

Hawa kaka zake Joshua wakituonyesha sehemu wanayolala pamoja na joshua wakati mama huyo yeye amesema  yeye huwa analala na joshua chumbani kwake 

Baadhi ya majirani wakisimulia mkasa huo

Amini usiamini mtoto Joshua baada ya kuona mkeka mzuri alijilaza kwa furaha kwani amezoea kulala sakafuni

Mama mlezi wa Joshua akijiandaa kumpeleka joshua kituo cha afya akapate matibabu baada ya kuamriwa kufanya hivyo




Habiba Ibrahimu amesema kuwa tukio la kufungiwa ndani mtoto ni la aibu kubwa hivyo halipaswi kufumbiwa macho na jamii husika hivyo ametaka hatua za haraka zichukuliwe ili kuokoa maisha ya mtoto huyo. (Picha na Ezekiel Kamanga.)

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mtoto mwenye umri wa zaidi ya miaka miwili amefungiwa ndani na wazazi wake kwa kipindi cha miaka miwili sasa bila kutoka nje pamoja na kukosa matunzo muhimu hali ambayo imepelekea mtoto huyo kudhoofu kiafya.

Tukio hilo limetokea leo jijini mbeya katika  mtaa wa Ikuti kata ya Iyunga ambapo majirani wa karibu na mtoto huyo pamoja na baadhi ya viongozi wa mtaa huo kufika nyumbani anapoishi mtoto huyo kwa lengo la kufahamu maendeleo yake .

Mtoto huyo amefahamika kwa jina la Joshua Joseph umri unao kadiriwa  kuwa ni kati ya miaka miwili au mitatu  ambaye alikutwa nyumbani hapo akiwa pekee yake huku wazazi wake wakiwa wameondoka kuelekea kwenye shughuli zao .



Akizungumzia tukio hilo Kaimu barozi wa mtaa huo wa Ikuti Ndugu Aloni Mboya amesema kuwa hali hiyo imenza kujitokeza kwa kipindi cha miaka mitatu sasa hali ambayo imepelekea mtoto huyo kukumbwa na maradhi ya utapiamlo.



Amesema katika kipindi cha mwaka 2011 mwezi wa tatu alipokea  taarifa kuhusiana na   suala hilo  ambapo baba wa mtoto huyo ndugu Joseph Simoni aliitwa katika ofisi za mtaa kwa lengo la kumhoji juu ya malezi ya mtoto huyo.

 Aidha baada ya kuhojiwa alikiri kosa ambapo alipewa onyo na viongozi wa mtaa ambao walimtaka kuhakikisha anamtunza vema mtoto huyo kwa kumpatia chakula bora  pamoja na huduma nyingine.

.
Mara baada ya mtu huyo kupewa kalipio na viongozi wa mtaa hali hiyo iliendelea tena ambapo wao kama viongozi wa shina pamoja na wananchi walimuita yeye pamoja na mke wake aitwaye  Sekera Watsoni (40) kuhama mtaani hapo kwa kwa kipindi cha miezi sita ambapo walikaidi agizo hilo.

 Amesema mara baada ya watu hao kugoma waliamua kuwaacha na kuwaondoa katika umoja wa ubarozi wao na kuto watambua tena kama wananchi wa eneo hilo kutokana na vitendo vyao vya kikatili dhidi ya mtoto huyo.

Kwa upande wao Maafisa maaendeleo ya jamii kata ya Igawilo na Iyunga ambao ndio waliofika katika eneo hilo wamesema kuwa matukio kama hayo yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara ndani ya jamii hasa kwa vitendo vya kunyanyaswa kwa watoto wanawake.

Mmoja wa Maafisa hao Ndugu Habiba Ibrahimu amesema kuwa tukio la kufungiwa ndani mtoto ni la aibu kubwa hivyo halipaswi kufumbiwa macho na jamii husika hivyo ametaka hatua za haraka zichukuliwe ili kuokoa maisha ya mtoto huyo
  
Amesema hali ya kiafya ya mtoto si ya kulizisha kutokana na kusumbuliwanna maradhi mbalimbali yanayotokana na kukosekana kwa lishe bora pamoja na huduma nyingine.

Amesema anawashukuru majirani pamoja na viongozi wengine wa serikali ya mtaa ambao wamekuwa karibu na mtoto huyo kwa kipindi chote cha miaka miwili licha ya kutokuwepo kwa ushirikiano toka kwa  wazazi wa mtoto ambaye kwa sasa amefikishwa katika kituo cha afya  Inyala Kata ya Iyunga  jijini hapa.

Awali inaelezwa kuwa baba na mama wa mtoto huyo  wamekwisha tengana kwa kipindi kirefu sasa kutokana na kutokuwepo kwa maelewano ndani ya nyumba hiyo hali ambayo ilimfanya baba huyo kuoa mwanamke mwingine ambaye ndiye anaye ishi na mtoto kwa sasa kama mama wa kambo.

Amesema kutoka na kuwepo kwa mgawanyiko huo ndani ya familia baba pamoja na mama huyo ambaye ni mke wa pili walichukua jukumu la kuishi na watoto wote walio achwa na mwanamke wa kwanza ambapo kwa asilimia kubwa ndiko kuliko sabababisha kuwepo kwa hali hiyo ya manyanyaso ya mtoto.

Hata wakati wa tukio hilo la kumtoa mtoto huyo ndani baba mzazi wa mtoto hakuwepo katika maeneo hayo ya nyumbani ambapo maafisa ustawi wa jamii pamoja na majirani waliamua kuchukua jukumu la kumpeleka mtoto huyo katika kituo cha afya Inyala kilichopo Kata ya Iyunga kwa lengo la kumfanyia uchunguzi na kutambua nini kinacho msumbua mtoto huyo
 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger