Pages


Home » » Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dk. Hussein Mwinyi amezindua kipimo cha malaria.

Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dk. Hussein Mwinyi amezindua kipimo cha malaria.

Kamanga na Matukio | 02:04 | 0 comments


Dk. Mwinyi akihutubia.
Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dk. Hussein Mwinyi amezindua kipimo cha malaria kinachotoa majibu ya haraka katika vituo binafsi vya kutolea huduma za afya.


Kipimo hicho ambacho tayari kinafanya kazi katika vituo vya afya vya serikali, kinatoa majibu kwa muda wa dakika 15 tangu mgonjwa kuanza kutolewa damu.


Akiongea katika uzinduzi huo, Dk Mwinyi amesema kuzinduliwa kwa kipimo hicho kinachojulikana kama MRDT wana lengo la kupambana na Malaria na kusogeza huduma kwa wananchi wote kwa gharama nafuu.


Dk. Mwinyi amewataka wananchi kuacha tabia ya kutumia dawa za malaria bila kupima hata kama utakuwa na dalili za homa badala yake mgonjwa afike katika kituo cha afya kilicho karibu yake kwa uchunguzi zaidi. 


Ameongeza kuwa gharama ya kupima kwa kipimo hicho haitakiwi kuzidi shilingi 1,100 na kwamba serikali imejipanga vizuri kuwadhibiti watoa huduma wa afya wa sekta binafsi watakaozidisha bei kinyume na maelekezo ya serikali.


Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha uchunguzi na tiba ya malaria katika mpango wa taifa wa kudhibiti malaria nchini Dk. Sigsbert Mkude amesema kipimo hicho kimefanyiwa utafiti wa kina na kuonekana kuwa kinafa japo kuna baadhi ya changamoto kwa baadhi ya wagonjwa.


Kutokana na taarifa ya utafiti katika jamii THMIS katika kipindi cha miaka mitano, maambuki ya ugonjwa wa malaria yamepungua kwa zaidi ya asilimia 50 kutoka asilimia 18 mwaka 2007/2008 hadi asilimia 9 mwaka 2011/2012.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger