Pages


Home » » Bajeti; Bia, Sigara, Vinywaji Vikali Bei Juu,

Bajeti; Bia, Sigara, Vinywaji Vikali Bei Juu,

Kamanga na Matukio | 02:30 | 0 comments
Photo: Bajeti; Bia, Sigara, Vinywaji Vikali Bei Juu







Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk William Mgimwa.
Dar es Salaam, Tanzania. Serikali imeoongeza kodi kwenye magari makuukuu, bia, vinywaji vikali, na baridi ambavyo kodi imekuwa ikiongezwa kila mwaka na kuwathiri watumiaji.


Kutokana na hali hiyo wanywaji pombe na sigara watalazimika kutumia fedha nyingi ili kupata huduma hizo.


Bidhaa zisizokuwa za mafuta ambazo zimefanyiwa marekebisho na kuongezwa kodi ni mvinyo, pombe, vinywaji vikali, na sigara. Vinywaji hivyo vimeongezwa kodi kwa asilimia 10. 


Kutokana na bajeti ya mwaka 2013/14 iliyosomwa jana bungeni na Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk William Mgimwa, Vinywaji vikali vimepanda kutoka Sh2,392 hadi Sh2,631 kwa lita sawa na ongezeko la Sh239 kwa lita moja.


Bia inayotengenezwa kwa nafaka nchini ambayo haijaoteshwa imeongezwa kodi kutoka Sh310 kwa lita hadi Sh341 kwa lita, sawa na ongezeko la Sh31 kwa lita.


Pia bia nyingine zote zimepanda kutoka Sh525 kwa lita hadi Sh578 kwa lita sawa na ongezeko la Sh51 kwa lita.


Kwa upande wa vinywaji baridi, vimeda kutoka Sh83 kwa lita hadi Sh91 kwa lita sawa na Sh na ongezeko la Sh8 kwa lita.


Vile vile sigara zenye kichungi na zinazozalishwa nchini zimepanda kwa asilimia 75, kutoka Sh19,410 hadi Sh21, 351 kwa sigara 1,000 sawa na ongezeko la Sh1.94 na senti 94 kwa sigara moja.




Ushuru pia umeongezwa kwenye magari yasiokuwa ya uzalishaji na yenye umri wa miaka 10 kutoka asilimia 20 mpaka hadi asilimia 25.


Dk Mgimwa alisema hatua hiyo imelenga kupunguza uagizaji wa magari chakavu ili kulinda mazingira na kupunguza ajali za mara kwa mara.


Uamuzi wa serikali kuongeza kodi katika maeneo hayo na mengine, utaisaidia serikali kuongeza mapato ya Sh510 bilioni.

Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk William Mgimwa.
Dar es Salaam, Tanzania. Serikali imeoongeza kodi kwenye magari makuukuu, bia, vinywaji vikali, na baridi ambavyo kodi imekuwa ikiongezwa kila mwaka na kuwathiri watumiaji.


Kutokana na hali hiyo wanywaji pombe na sigara watalazimika kutumia fedha nyingi ili kupata huduma hizo.


Bidhaa zisizokuwa za mafuta ambazo zimefanyiwa marekebisho na kuongezwa kodi ni mvinyo, pombe, vinywaji vikali, na sigara. Vinywaji hivyo vimeongezwa kodi kwa asilimia 10. 


Kutokana na bajeti ya mwaka 2013/14 iliyosomwa jana bungeni na Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk William Mgimwa, Vinywaji vikali vimepanda kutoka Sh2,392 hadi Sh2,631 kwa lita sawa na ongezeko la Sh239 kwa lita moja.


Bia inayotengenezwa kwa nafaka nchini ambayo haijaoteshwa imeongezwa kodi kutoka Sh310 kwa lita hadi Sh341 kwa lita, sawa na ongezeko la Sh31 kwa lita.


Pia bia nyingine zote zimepanda kutoka Sh525 kwa lita hadi Sh578 kwa lita sawa na ongezeko la Sh51 kwa lita.


Kwa upande wa vinywaji baridi, vimeda kutoka Sh83 kwa lita hadi Sh91 kwa lita sawa na Sh na ongezeko la Sh8 kwa lita.


Vile vile sigara zenye kichungi na zinazozalishwa nchini zimepanda kwa asilimia 75, kutoka Sh19,410 hadi Sh21, 351 kwa sigara 1,000 sawa na ongezeko la Sh1.94 na senti 94 kwa sigara moja.





Ushuru pia umeongezwa kwenye magari yasiokuwa ya uzalishaji na yenye umri wa miaka 10 kutoka asilimia 20 mpaka hadi asilimia 25.


Dk Mgimwa alisema hatua hiyo imelenga kupunguza uagizaji wa magari chakavu ili kulinda mazingira na kupunguza ajali za mara kwa mara.


Uamuzi wa serikali kuongeza kodi katika maeneo hayo na mengine, utaisaidia serikali kuongeza mapato ya Sh510 bilioni.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger