Pages


Home » » Shirika la viwango Tanzania TBS limepiga marufuku biashara ya uuzwaji wa nguo za ndani za mitumba zinazoingizwa kwenye soko la hapa nchini.

Shirika la viwango Tanzania TBS limepiga marufuku biashara ya uuzwaji wa nguo za ndani za mitumba zinazoingizwa kwenye soko la hapa nchini.

Kamanga na Matukio | 03:58 | 0 comments
Shirika la viwango Tanzania TBS limepiga marufuku biashara ya uuzwaji wa nguo za ndani za mitumba zinazoingizwa kwenye soko la hapa nchini.

Msemaji wa shirika la viwango TBS Bi. Rhoida Andusamile amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa matakwa ya agizo la sheria ya 2009 inayozuia matumizi ya nguo za ndani zilizokwisha tumika.

 Lakini licha ya unafuu wa gharama za upatikanaji wa nguo za mitumba Nchini, Serikali kupitia TBS imepiga marufuku biashara ya uuzwaji wa nguo hizo ikiwemo soksi na nguo za kulalia zoezi linalohusisha Nchi nzima.

Mara nyingi nguo za ndani za mitumba zimekuwa zikitumiwa na jinsia zote mbili lakini wanawake ndiyo wameonekana kuwa wateja wakubwa wa nguo hizo wao walikuwa na maoni gani juu ya kupigwa marufuku uuzwaji wa ngao hizo?.

Kwa upande wao wauzaji wa nguo hizo walikuwa na maneno ya kuongea "Hii ni mara ya pili kwa Shirika la viwango Tanzania - TBS kupiga marufuku biashara ya uuzwaji wa nguo za ndani za mitumba, lakini bado biashara hiyo imekuwa ikishamiri kwa kasi".

 #source-Star Tv#
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger