Pages


Home » » WANAWAKE WAMETAKIWA KUJITOKEZA KUPIMA AFYA ZAO ILI KUEPUKANA NA UGONJWA WA SHINGO YA KIZAZI

WANAWAKE WAMETAKIWA KUJITOKEZA KUPIMA AFYA ZAO ILI KUEPUKANA NA UGONJWA WA SHINGO YA KIZAZI

Chimbuko Letu | 07:49 | 0 comments
 Picha hii imetumika kupamba habari, lakini haijachukuliwa katika eneo husika la habari hii.
 
 
Na Ezekiel Kamanga.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ileje Mkoani Mbeya Daktari Gerald Yubaha amewataka wanawake kujitokeza kwa wigi katika zahanati,vituo vya Afya na Hospitali ili kupima afya zao ili kubaini na kuondoa ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi Wilayani humo.

Yubaha ameyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani iliyofanyika Kiwilaya katika Hospitali ya Wilaya iliyopo Itumba Mei 12 mwaka huu ambapo Wauguzi na wahudumu wa Afya walifanya maandamano ya kumkumbuka Muuguzi wa kwanza Duniani ambapo maandamano hayo yalipokelewa na Mkuu wa Wilaya Rosemary Senyamule.

Kaimu Mganga Mkuu amesema kuwa baadhi ya changamoto ni pamoja na ukosefu wa mashine za kupimia vipimo katika Wilaya ambazo zingebaini magonjwa mbalimbali yakiwemo ya shingo ya uzazi kwa akina mama kwani kwa sasa huduma hiyo huipata katika hospitali ya wazazi Meta iliyopo Jijini Mbeya na Hospitali yake hutumia gharama kubwa kuwasafirisha wagonjwa wanaowabaini.

Tangu kuanza kutolewa elimu ya ugonjwa wa shingo ya uzazi wagonjwa wanne walibainika na ugojwa huo ambapo wawili kati yao walifariki kutokana na kuchelewa kupata matibabu na wawili walisafirishwa hadi Mbeya ambapo wanapatiwa matibabu katika Hospitali ya Wazazi ya Meta.

Katika maandamano wauguzi hao walibeba mabango mbalmbali ili kufikisha ujumbe kwa serikali ambayo baadhi yakidai malimbikizo ya stahiki mbalimbali wanazodai watumishi wa sekta ya Afya ambayo hayajalipwa kwa muda mrefu.

Akijibu kero hizo za Wauguzi Mkuu wa Wilaya alisema Serkali imejitahidi siku hadi siku kuhakiksha wanalipa malimbikizo yao kwa wakati kadri fedha zinapopatikana kwani serikali haipo tayari haipo tayari kuona watumishi wake wanaishi maisha duni.

Alisema Serikali ina majukumu mengi ikiwa ni pamoja na upanuzi wa Hospitali hiyo ambapo ujenzi unaendelea ili kuwaondolea adha ya wananchi wa wilaya hiyo badala ya kusfiri umbali mrefu na wengi hupoteza maisha kwa kukosa gharama za kuwasafirisha ndugu zao wanapokuwa wanahitaji matibabu zaidi Mbeya.

Aliwataka kuendelea kuwa wavumilvu na kuwapongeza kwa moyo wa uzalendo ambao wamekuwa wakifanya wa kutoa huduma licha ya kufanya kazi katika mazingira magumu na kuwajali wagonjwa wanaofika hosptalini kwa ajili ya kupata huduma.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger