Pages


Home » » Halmashauri ya Jiji la Mbeya yaombwa kuweka kipaumbele katika kuboresha huduma za kijamii.

Halmashauri ya Jiji la Mbeya yaombwa kuweka kipaumbele katika kuboresha huduma za kijamii.

Chimbuko Letu | 08:50 | 0 comments
Na Ezekiel Kamanga.
Wananchi wanaotumia kivuko cha Daraja la Makaburi ya Sabasaba Mtaa wa Jakaranda wameiomba halmashauri ya Jiji la Mbeya kuweka kipaumbele katika kuboresha huduma za kijamii  hususani miundombinu ya barabara, vivuko  kwani vingi vimekuwa hatarishi katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha Jijini hapa.

Wakizungumza na kituo hiki jana  kwa nyakati tofauti  walisema kuwa kivuko hicho kimekuwa chakavu kwa muda sasa licha ya kutoa taarifa  kwa viongozi wa serikali za mitaa.

Athanas Amosy,Mkazi wa Forest alisema ni vema halmashauri ikaliona hili na kulifanyia kazi kwani wananchi wengi  wamekuwa wakitegemea kivuko  hichi ambacho ni muhimu kwetu kwa shughuli mbalimbali za kiofisi na hata wafanyabishara kwani kimekuwa tishio pindi mvua zinapokuwa zikinyesha.

Mkazi wa Magereza Salome Adamson ,alisema wanaiomba  Serikali kuangalia namna ya kuboresha  miundombinu rafiki inayotumika na wananchi kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi katika maeneo ya mijini .

Akizungumza na gazeti hili ,Mwenyekiti wa Mtaa wa sabasaba Aidan Ng'oma alikiri kuwepo kwa changamoto hizo na kwamba alituma maombi   halmashauri  na kwamba uwenda ni miongoni mwa  miradi itakayoboreshwa kwa mwaka huu wa fedha .

"Kwani mkakati sio kuboresha kivuko hiki pekee  kipo kingine korofi katika eneo la ujenzi ambacho  ni miongoni vya vitakavyofanyiwa ukarabati"alisema.

Kwa upande wake ,Diwani wa kata ya Mbalizi Road,Adam Hussein alipohojiwa kuhusiana na malalamiko ya wananchi alisema kuwa  alikwisha wasilisha kwenye vikao vya baraza la madiwani na kwamba miongoni mwa  miradi iliyoingizwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/17 .

"Tayari halmashauri imetenga  fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata yangu ikiwa ni pamoja na kuboresha vivuko,miundombinu ya barabara korofi "alisema.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger