Pages


Home » » WANYANYASAJI WA WATOTO WAANZA KUCHUKULIWA HATUA MKOANI MBEYA.

WANYANYASAJI WA WATOTO WAANZA KUCHUKULIWA HATUA MKOANI MBEYA.

Chimbuko Letu | 07:40 | 0 comments



JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mwanamke mmoja Mwanahawa Nasoro(32) Mkazi wa Mtaa wa Airport Kata ya Iyela Jijini Mbeya akituhumiwa kumfanyia vitendo vya unyanyasasaji Mtoto wa ndugu yake.
 
Mwanamke huyo anatuhumiwa kumtesa, mtoto John Msumba(3) ambaye ni Shangazi yake baada ya kumfungia ndani kumnyima chakula na kumpa kipigo kikali kilichompelekea kuwa na majeraha mwilini mwake pamoja na maumivu makali yaliyosabisha kulazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kwa matibabu zaidi.
 
Akizungumza na Mtandao huu, Mjumbe wa Mtaa wa Airport, Rehema Mohammed alisema kuteswa na kukamatwa kwa Mwanamke huyo kuligundulika Machi 12, Mwaka huu majira ya saa nne asubuhi kufuatia kuwepo kwa msiba jirani na nyumba yake.
 
Alisema wakati watu wako msibani na mlango wa nyumba ya Mwanamke huyo ukiwa umefungwa na kufuli kwa nje ilisikika sauti ya Mtoto akilia ndani jambo ambalo liliwashangaza wengi ndipo alipotoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Mtaa Enock Mwampagama ambaye pia alitoa taarifa kwa Mtendaji wa Mtaa aliyelitaarifu Jeshi la Polisi.
 
Alisema baada ya Mwanamke huyo kubanwa alikiri kuwepo kwa Mtoto ndani na kwamba alikuwa akimfanyia hivyo kutokana na tabia yake ya kujisaidia haja kubwa hovyo hali iliyokuwa imemchosha na kuamua kumpa adhabu kama hiyo.
 
Alipoulizwa kuhusiana na wazazi wa Mtoto huyo alidai kuwa hafahamu mahali alipo mama mzazi na kuongeza kuwa baba yake aliyefahamika kwa jina la Sumba Dinda kuwa yupo machimboni Wilayani Chunya kwenye Migodi ya Dhahabu.
 
Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa Mwanamke huyo anashikiliwa hadi hapo Afya ya mtoto ambaye ni mhanga wa Tukio hilo itakapoimarika ndipo atakapofikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili.
 
Wakati huo huo baadhi ya Wasamaria wema wameziomba taasisi zinazoshughulikia masuala ya unyanyasaji wa kijinsia na watoto zikiwemo Mtandao wa Waandishi wa habari Wanawake na Jinsia (TAMWA) na Taasisi ya Jinsia (TGNP) kuingilia kati maswala hayo ili kukomesha vitendo hivyo katika jamii.
 
Aidha baadhi ya wasamaria wema wajitokeza kuchangia fedha za matibabu ya mtoto huyo yanayoendelea katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya baada ya mmoja wa Waandishi wa Mtandao huu ambaye pia ni Mtangazaji wa Kituo cha Redio cha Bomba cha Jijini Mbeya kuendesha harambee fupi katika kipindi chake na kufanikiwa kukusanya shilingi 35,000/= zilizotumika kununulia madawa.
 
Mbali na hilo TAMWA inaombwa kushughulika moja kwa moja na mtoto huyo ili kuhakikisha haki inapatikana ikiwa ni pamoja na kupiga vita unyanyasaji wa kijinsia uliokithiri ndani ya jamii kutokana na juhudi ziliooneshwa na mtandao huo katika kukabiliana na hali hiyo kwa kutoa Elimu kwa wanahabari mara kwa mara katika kuibua vitendo hivyo na kuvikemea.


Na Ezekiel Kamanga.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger