Pages


Home » » VIONGOZI WA CHAMA CHA MAPINDUZI WATAKIWA KUWA KARIBU NA WANANCHI.

VIONGOZI WA CHAMA CHA MAPINDUZI WATAKIWA KUWA KARIBU NA WANANCHI.

Chimbuko Letu | 23:46 | 0 comments
Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM Dr, Jakaya Kikwete akiinua jembe na nyundu kwa maana ya nembo ya chama hicho mara baada ya kuingia uwanjani.

Jakaya Kikwete alipokuwa akianza kutoa hotuba mara baada ya kuingia katika uwanja huo.

baadhi ya viongozi wa chama hicho wakimshangilia mwenyekiti Jakaya Kikwete alipokuwa akiingia uwanjani.

Raisi Kikwete alipokuwa akiingia katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine kwaajili ya maadhimisho hayo.
............................................................................................................


Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Dr, Jakaya Mrisho Kikwete amewataka viongozi na wanachama wa chama hicho, kuwa karibu na wananchi kwa lengo la kusikiliza matatizo ya wananchi na kuyatatua, kwakufanya hivyo itakuwa chachu ya wananchi kukiamini chama.

Kikwete ameyasema hayo alipokuwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 37 tangu kuanzishwa kwake yaliyofanyika leo katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini  Mbeya.
Kikwete amesema kumekuwa na tabia kwabaadhi ya viongozi wa chama hicho kutotatua matatizo ya wananchi pindi wanapopewa taarifa kuhusu kero hizo.

Aidha Kikwete amempongeza katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana kwakufanya ziara katika mikoa ya nyanda za juu kusini iliyoleta mafanikio  makubwa katika cha hicho.

Amesema Kinana katika ziara yake alikuwa akisikiliza matatizo ya wananchi na kuyatafutia ufumbuzi, pia amekuwa nao wananchi bega kwa bega katika Nyanja mbali mbali.

Pia Kikwete amesema mpango wa chama cha Mapinduzi ni kuboresha maisha ya watanzania katika sekta mbali mbali ikiwa pamoja na maji, umeme, elimu afya na miundombinu.


Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger