Pages


Home » » TCRA YAWAFUNDA WAANDAAJI WA VIPINDI NA WATANGAZAJI WA REDIO KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI.

TCRA YAWAFUNDA WAANDAAJI WA VIPINDI NA WATANGAZAJI WA REDIO KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI.

Chimbuko Letu | 08:51 | 0 comments
Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Tcra ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi, Magreth Mnyagi amesema lengo la washa hiyo ni kuwakumbusha watangazaji kuhusu kufuata maudhui yaliyokusudiwa yanayoelimisha na kuburudisha jamii na kuwa chachu ya maendeleo ya uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Mgeni rasmi wa Washa hiyo, Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Mbeya, Leonard Magacha ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro amesema kukiuka kwa maadili katika baadhi ya vituo vya utangazaji kunatokana na wamiliki kuwaajiri wafanyakazi wasiokuwa na taaluma ya Utangazaji.




Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) Kanda ya Mbeya MhandisDeogratius Moyo wana warsha kuchangia mada

Frederick  Ntobi Naibu Mkurugenzi idara ya utangazaji Mamlaka ya mawasiliano akiwafunda waandaaji wa vipindi  na watangazaji wa radio kanda ya nyanda za juu kusini


Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy akiongoza mijadala katika Warsha ya Siku Mbili kwa kwa waandaaji wa vipindi na watangazaji wa Radio



Baadhi ya watangazaji wakichangia mada


Picha ya pamoja



MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) inaendesha warsha ya Siku mbili kwa Wandaaji wa Vipindi vya Redio pamoja na watangazaji kutoka Mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, inayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mkapa uliopo Sokomatola Jijini Mbeya.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Warsha hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Tcra ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi, Magreth Mnyagi amesema lengo la washa hiyo ni kuwakumbusha watangazaji kuhusu kufuata maudhui yaliyokusudiwa yanayoelimisha na kuburudisha jamii na kuwa chachu ya maendeleo ya uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Amesema vipo vituo vingi ambavyo vimekiuka maudhui yaliyokusudiwa ambayo hayazingatii maadili ya Tanzania na kupelekea uvunjifu wa amani kutokana na kutangaza vitu vinavyokiuka maudhui waliyopewa, hivyo kupitia Washa hiyo itasaidia kuwakumbusha kufuata misingi taratibu na kanuni za utangazaji.

Kwa upande wake Mgeni rasmi wa Washa hiyo, Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Mbeya, Leonard Magacha ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro amesema kukiuka kwa maadili katika baadhi ya vituo vya utangazaji kunatokana na wamiliki kuwaajiri wafanyakazi wasiokuwa na taaluma ya Utangazaji.

Magacha amesema shida iliyopo ni kwa wamiliki wa Vyombo vya habari ambao huajiri watu wasiokuwa na taaluma kwa kuogopa kulipa hivyo kutafuta watangazaji wa kuokoteza ambao ndiyo chanzo cha kukiuka Maudhui.

Aidha katika Washa hiyo washiriki waliweza kufundishwa kuhusu Masharti na sheria ya Leseni( Licence conditions and Code of Conduct), Kanuni za Utangazaji pamoja na kutazama DVD mbali mbali zenye makosa kwenye vipindi vya baadhi ya Televisheni na Redio ambapo washiriki walipata muda wa kujadili.

Na Mbeya yetu
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger