
Rais Jakaya Mrisho Kikwete
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Mheshimiwa Jakaya
Mrisho Kikwete ameshtushwa na kuhuzunishwa sana na tukio la kushambuliwa
na kuuawa kwa vijana saba hodari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania
waliokuwa wanalinda amani katika eneo la Darfur, Sudan.
Kwa hakika, Rais amesikitishwa
sana na kitendo hicho ambako wanajeshi wengine 14 wa Tanzania
wamejeruhiwa...