Pages


MTOTO AFARIKI BAADA YA KUSHAMBULIWA NA KUNDI LA NYUKI.

Kamanga na Matukio | 03:35 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbozi. Mtoto Runi Fabi(5) mkazi wa Kitongoji cha Namleya,Ilembo,Kata ya Vwawa,Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya amefariki dunia baada ya kushambuliwa na kung'atwa na kundi la nyuki. Tukio hilo limetokea Mei 27 mwaka huu majira ya saa sita mchana,wakati akicheza na watoto wenzake nje kidogo ya nyumba yao. Balozi wa mtaa huo Bwana Hanzi Wega, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kubainisha ya kwamba tukio hilo ni la pili kutokea mtaani kwake. Ameongeza kuwa mwezi Mei mwaka jana mwanamke marehemu Namyugumbi Nzunda, aliuawa baada ya kuvamiwa na kundi la nyuki. Hata hivyo Baba mzazi wa mtoto huyo Bwana Fabi Mjewa amesema alishangaa kuletewa mwanae...

WATU WATATU WASHTAKIWA KWA KUJERUHI.

Kamanga na Matukio | 03:34 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya. Watu watatu wakazi wa Tuduma Kati, Wilaya mpya ya Momba, Mkoani Mbeya wameshtakiwa kwa tuhuma za kujeruhi. Watuhumiwa hao ni pamoja na Martha Ndabila(30),Gibe Prosper(37) na Victor Haonga(37) ambapo wote kwa pamoja walifikishwa katika Mahakama ya mwanzo Tunduma Mei 29 mwaka huu. Watuhumiwa hao walifikishwa mbele ya Hakimu Leonard Kazimzuri wa mahakama hiyo, wakidaiwa kumjeruhi Bwana Elias Cheyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mamlaka ya Halmashauri ya mji mdogo wa Tunduma, Mei 28 mwaka huu majira ya saa 5:30 asubuhi. Akisoma mashtaka mbele ya mahakama hiyo PP Nathani amesema kuwa watu hai wametenda kosa la jinai kifungu cha 241 sura ya 16 ya...

WAUMINI WA EAGT KANDETE WAMTUHUMU MCHUNGAJI KWA USHIRIKINA.

Kamanga na Matukio | 05:34 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.  Waumini 45 wa kanisa la EAGT(Evangelical Asemblies of God), Kandete Mwakaleli, Wilaya ya Rungwe,Mkoani Mbeya wameamua kujitenga na kanisa hilo lililopo chini ya Mchungaji Jaremia Mwamwaja wa kanisa hilo kwa tuhuma za ushirikina. Sakata hilo limetokea Mei 27 mwaka huu katika ibada ambapo mtoto wa Mchungaji huyo aitwaye Lydia Mwamwaja kupanda madhabauni na kushuhudia kuwa yeye anajihusisha na ushirikina ndipo waumini haowalipotaharuki na kumwamuru mchungaji huyo aondoke kanisani hapo na familia yake lakini mchungaji alikataa. Alipopekuliwa mtoto huyo wa mchungaji alikutwa na hirizi mkono wa kushoto, ambapo alikiri kuwa yeye anajihusisha na masuala...

WATU WAWILI WAMEFARIKI KATIKA MAZINGIRA MAWILI TOFAUTI.

Kamanga na Matukio | 05:19 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya. Watu wawili wamefariki Mkoani Mbeya katika matukio mawili tofauti, likiwemo la mtoto kufariki baada ya kutumbukia mtoni wakati akicheza na wenzake. Tukio hilo la mtoto huyo aitwaye Alfa Sadiki(2),limetokea katika Kijiji cha Lukululu,Wilaya ya Mbozi Mei 26 mwaka huu majira ya saa sita mchana. Baba mzazi wa mtoto huyo Bwana Sadick Eliakimu Swajiamesema wakati tukio yeye alikuwa amesafiri kuelekea Tunduma. Tukio jingine limetokea Kijiji cha Mbuyuni,Kata ya Mbuyu,Wilaya ya Chunya Salome Herman(20) alifariki dunia baada ya kupigwa na jiwe,alipokuwa akipitia njiani Mei 26 mwaka huu majira ya saa tatu usiku. Katika tukio hilo Bwana Joseph Mwandyehe alikuwa...

MWENYEKITI NA MKEWE WASABABISHA WANANCHI KUSUSIA MKUTANO.

Kamanga na Matukio | 04:55 | 0 comments
Mke wa Mwenyekiti wa Kijiji wa Kijiji cha Motomoto Bi Salome Ipopo aliyeketi, ikiwa amekwepa kamera, ambaye alivuruga mkutano kwa kuporomosha matusi kwa kila mwananchi aliyekuwa akichangia hoja katika mkutano wa hadhara baada ya mumewe kutuhumiwa kuuza ardhi ya kijiji na kufuja pesa za mradi wa maji. Wananchi wa Kijiji cha Motomoto wakielekea katika mkutano wa hadhara wa kijiji hicho. Wananchi walioitikia wito wakiwa wameshikwa na butwaa...

MKE WA MWENYEKITI AVURUGA MKUTANO WA KIJIJI CHA MOTOMOTO, BAADA YA MUMEWE KUWEKWA KITIMOTO.

Kamanga na Matukio | 04:42 | 0 comments
Mke wa Mwenyekiti wa Kijiji wa Kijiji cha Motomoto Bi Salome Ipopo aliyeketi, ikiwa amekwepa kamera, ambaye alivuruga mkutano kwa kuporomosha matusi kwa kila mwananchi aliyekuwa akichangia hoja katika mkutano wa hadhara baada ya mumewe kutuhumiwa kuuza ardhi ya kijiji na kufuja pesa za mradi wa maji.(Picha na Ezekiel Kamanga). ***** Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya. Mke wa Mwenyekiti wa Kijiji wa Kijiji cha Motomoto Bi Salome Ipopo amevuruga...

VIONGOZI WAJIMILIKISHA ARDHI WILAYA YA MBARALI.

Kamanga na Matukio | 03:31 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbarali. Viongozi 7 wa Kijiji cha Itamba, Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya wanatuhumiwa kuuza ardhi ya kijiji hicho kwa wafanyabiashara na wao kujimilikisha sehemu kubwa ya ardhi hiyo kinyume na makubaliano. Hayo yamebaika baada ya kutembelea Kijiji hicho na kukutana na wananchi zaidi ya 200, ambao wameulalamikia uongozi wa kijiji hicho. Viongozi waliotajwa na Mwenyekiti wa Kijiji Bwana Venance Magiye ambaye anadaiwa kumiliki hekari 35, Afisa Mtendaji wa kijiji Bwana Damson Simasilya hekari 10, Mwenyekiti wa ulinzi Bwana Ally Mpwaga hekari 20, Mjumbe Bwana Aidan Sangula hekari 60. Wengine ni Bwana Amir Mlamata hekari 20, Majulisho Mwandungu hekari 30 na Jackson...

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBEYA VIJIJINI YAITELEKEZA SHULE iILIYOGHARIMU MIL 80.

Kamanga na Matukio | 03:05 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya. Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mkoani Mbeya imeitelekeza Shule ya Sekondari Galijembe yenye Kidato cha tano na sita, iliyopo Kata ya Tembela wilayani humo. Hayo yamebainishwa na wananchi baada ya mtandao huu kutembelea shule hiyo na kukuta vyumba vya madarasa yapatayo nane yaliyojengwa kwa nguvu zao, ambapo Serikali haijatoa chochote katika ujenzi huo wa shule hiyo. Katika uchunguzi huo imebainika kuwa ni zaidi ya miaka 7 halmashauri imeitelekeza shule hiyo ya kisasa iliyojengwa kwa matofali ya saruji, kuezekwa kwa mabati na vyoo vya kisasa, kwa madai kuwa inaichukua shule hiyo kutoka mikononi kwa wananchi hao kwa lengo ya kuiendeleza. Mtandao...

BREAKING NEWS:- Viongozi wajimilikisha ardhi Wilaya ya Mbarali.

Kamanga na Matukio | 05:17 | 0 comments
*Mwenyekiti ajimilikisha hekari 35 za ardhi, Afisa mtendaji wa kijiji hekari 20 na mwingine auziwa hekari 100. ****Endelea kufuatilia mtandao huu ili kupata taarifa kamili*...

BREAKING NEWS:- HALMASHAURI YA WILAYA YA MBEYA VIJIJINI YAKABIDHIWA SHULE YA SEKONDARI, YAITELEKEZA!!

Kamanga na Matukio | 05:14 | 0 comments
*Mbunge aingia mitini kuongea na wananchi. *Madarasa 8 yajengwa kwa nguvu za wananchi, ni zaidi ya miaka 5 hayajatumika. *Wakuu wa wilaya watatu wa ahidi bila utekeleza...

NAO WANAFURAHIA MAISHA KAMA WENGINE

Kamanga na Matukio | 05:09 | 0 comments
Nimewakuta kijiji kimoja hivi mbali lakini hata nikikutonya huwezifika. Wanatokea katika nyumba hii Na baadaye hujichanganya na wenzao katika maeneo haya nyakati za jioni.(Picha na Rashid Mkwinda)....

MTOTO AFA MAJI AKIJARIBU KUOKOA KANDAMBILI/YEBOYEBO.

Kamanga na Matukio | 05:08 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya. Mkazi wa Kitongoji cha Mwanjelwa, Kijiji cha Itaka, Kata ya Itaka, Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya Daniel Bahati Mgala (3) amefariki dunia katika kisima cha maji ya kufyatulia matofali. Tukio hili limetokea kijijini hapo Mei 23 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi wakati marehemu akiwa na mwenzake alikuwa akiifuata Yeboyebo moja iliyotupwa na mwenzie katika kisima hicho alipojaribu kuifuata alizama na kufa papo hapo baada ya kunywa maji hayo. Aidha mwenzake alipoona kazama alimwita mzazi Bahati Mgala na alipofika alikuta mwanae amekwishafariki ndipo alitoa kwa Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Bwana Nsinkini na Mwenyekiti Bwana Mwashilindi. Viongozi hao...

KAMANDA NYOMBI AFANYIWA SHEREHE YA KUAGWA NA MJATA NA APEWA UCHIFU.

Kamanga na Matukio | 05:49 | 0 comments
Pichani aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi(wa pili kulia), ambaye ametawazwa kuwa Chifu na kupewa jina la Chifu Mwalyembe, akishikana mkono na Chifu wa kabila la Wanyiha katika sherehe ya kumuaga zilizofanyika katika Uwanja wa monesho ya Nanenane maarufu kwa jina la Uwanja wa John B. Mwakangale jana. Kamanda Nyombi amehamishiwa makao makuu ya jeshi hilo Jijini Dar es salaam. Kamanda Nyombi akiwa...

MICHUANO YA NYOMBI CUP YAENDELEA MKOANI MBEYA

Kamanga na Matukio | 05:48 | 0 comments
Kikosi cha timu ya Forest, kilichoibuka na ushidi wa goli 3-1 dhidi ya timu ya Isanga katika mashindano ya Kombe la Nyombi, na kuibuka na ushindi wa goli 3-1, katika Uwanja wa Ruanda Nzovwe, Jijini Mbeya. Kikosi cha timu ya Isanga kilichofungwa goli 3-1 dhidi ya  timu ya Forest, jijini hapa. Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi wa mkoa wa Mbeya Bwana Adam Simfukwe akisalimiana na waamuzi wa mpambano huo katika ufunguzi...

KAMPENI ZA UCHAGUZI CHUO KIKUU CHA TEOFILO KISANJI (TEKU) ZAZINDULIWA RASMI.

Kamanga na Matukio | 05:45 | 1comments
*Wanawake wawili wajitokeza kugombea nafasi ya Urais na Makamu Rais. Habari na Ezekiel Kamanga. Kampeni za uchaguzi wa kumpata Rais wa Chuo kikuu cha Teku, zimezinduliwa rasmi jana katika ukumbi wa Mwasakafyuka huku wagombea wakinadi sera zao. Kampeni hizo zilizinduliwa na Dakta Mozes D, na kusimamiwa na mkufunzi wa chuo Bwana Alawi Mikidadi ambapo Mkurugenzi wa uchaguzi Bi Nyemba Joyce aliweka hadharani wagombea watakao wania viti vya...

RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE AMUAPISHA PROFESA MARK MWANDOSYA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM JANA.

Kamanga na Matukio | 05:19 | 0 comments
 Waziri wa nchi katika ofisi ya Rais asiye na Wizara maalum Profesa Mark Mwandosya akila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam jana asubuhi.Wapili kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.Na watatu kulia ni Karani wa Baraza la Mawaziri Bwana Gerson Mdemu. Profesa Mwandosya akipokea miongozo ya kazi baada ya kula kiapo Ikulu jana asubuhi. Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza...

AJIRA KWA WATOTO, JAMANI HII YOTE ANGALAU WAPATE CHOCHOTE NA KWENDA SHULE.

Kamanga na Matukio | 05:18 | 0 comments
Watoto hawa walikutwa Mtaa wa Mabatini Jijini Mbeya, wakijishughulisha na biashara ya uuzaji wa sambusa na maandazi, hii yote ni kuhakikisha angalau wanapata kiasi chochote cha fedha kitakachowawezesha kwenda shule na kiasi kingine kikisaidia matumizi ya nyumbani.(Picha nq Godfrey Kahango...

WATU WAWILI WAFARIKI KATIKA MATUKIO MAWILI YA AJALI MKOANI MBEYA.

Kamanga na Matukio | 05:17 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya. Watu wawili wamefariki dunia, katika matukio mawili ya ajali ya barabarani wilayani Mbarali na Rungwe, Mkoani Mbeya. Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa Advocate Nyombi amesema ajali ya kwanza iliyotokea katika Wilaya ya Mbarali, mei 20 mwaka huu majira ya saa 10 jioni barabara ya Mbeya/Iringa gari nambari T 536 APU likiwa na tela lenye nambari T 330 APD aina ya Scania. Gari hilo lilikuwa likitokea Jijini Dar es salaam kuelekea mkoani Mbeya likiendeshwa na dereva aitwaye Ismail Kiteve iliacha njia na kupinduka kisha kusababisha kifo chake. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya hiyo iliyopo Rujewa, na chanzo cha...

UCHAMBUZI WA KILIMO CHA TUMBAKU

Kamanga na Matukio | 05:17 | 0 comments
Habari na Ester Macha, Chunya. Zao la Tumbaku ni zao ambalo limekuwa likiwakomboa wananchi na hivyo kupunguza ukali wa maisha waliyonayo hasa maeneo ya vijijini ambako wananchi wake wamekuwa na maisha magumu,licha ya kuwakomboa wananchi pia hata serikali imekuwa ikiongeza mapato yake kupitia halmashauri zake za wilaya zinazolima zao hilo.Kilimo hicho cha Tumbaku kimekuwa kiingizia serikali dola za kimarekani 614.8 kutokana na ushuru unaotolewa baada ya mauzo ya zao hilo kwa wakulima. Kwa kutambua hilo serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha vyama vya ushirika ambavyo vimeundwa kwa lengo la kuwasaidia wakulima vinaboreshwa na hata kusaidia ili viweze kupata mikopo kutoka...

MIRADI 7 ILIYOGHARIMU MILIONI 407.3 YAFUNGULIWA WILAYANI MBARALI WAKATI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA.

Kamanga na Matukio | 05:58 | 0 comments
  Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Peter Pinda akiwasha Mwenge wa Uhuru kitaifa jana katika Uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine ulipo jijini Mbeya.  ********* Habari na Angelica Sullusi, Mbarali. Jumla ya miradi saba inayogharimu kiasi cha shilingi milioni 407.3 imefunguliwa na Kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa Kapteni Honest Mwanosa, katika Wilaya ya Mbarali ambapo shilingi milioni 102.6 zimechangiwa...

DC MBEYA ALITAKA JESHI LA POLISI KUFUATA MAADILI YA KAZI YAO.

Kamanga na Matukio | 05:58 | 0 comments
Na Kenneth Ngelesi, Mbeya Mkuu wa wilaya ya Mbeya Dr Noman Sigalla amelitaka jeshi la polisi kuacha kutumia ubabe na kutopendelea baadhi ya watu wa kada fulani katika kutekeleza majukumu yao kwani kufanya hivyo huchangia watu kutokuwa na imani na jeshi hilo na baadaye kutokea vurugu.   Rai hiyo alitoa na Mkuu huyo mpya wa wilaya mbele ya kamati ya ulinzi na usalama  ya wilaya wakati akikabidhiwa ofisi hiyo na mtangulizi wake aliyestaafu Evansi Balama ambapo  shughuli za makabidhiano  zilifanyika siku ya jumatano katika ofisi za Mkuu wa wilaya zilizopo Mbeya mjini.   Dr. Sigalla amesema kuwa kutokana na uzoefu wake kwamba baadhi ya...
Pages (14)1234567 Next
 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger