Pages


Mganga maarufu wa jadi aliyefamika kwa jina la Shija Ndula Jinan’gai kuamua kusalimisha matunguli yake katika Kanisa la Nyumba ya Maombi(House of Prayer Shield of faith) Pambogo Kata ya Iyela jijini Mbeya.

Chimbuko Letu | 08:21 | 0 comments


Mganga maarufu wa jadi aliyefamika kwa jina la Shija Ndula Jinan’gai(35)mkazi wa Mapogolo Kata ya Madibira Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya ameachana na kazi hiyo na kuamua kusalimisha matunguli yake katika Kanisa la Nyumba ya Maombi(House of Prayer Shield of faith) Pambogo Kata ya Iyela jijini Mbeya.


Shija Ndula mwenye familia ya Mke na watoto wanne ambaye sasa anafahamika kwa jina la Mussa Shija amesema ameitumikia kazi hiyo takribani miaka saba kabla ya kuamua kuachana na kazi hiyo  na kujiunga na Kanisa linaloongozwa na Mchungaji Isaya Laiser chini ya Kiongozi wake Mkuu Nabii Mulilege Mkombo maarufu(Mzee wa Yesu) kutokana na kutopata mafanikio katika uganga wa kienyeji.

Akiongea kwa ujasiri mganga huyo amesema kuwa kazi aliyokuwa akiifanya kwa muda wote huo hakupata mafanikio yoyote licha ya kutoza fedha nyingi kwa wateja wake kuanzia shilingi laki moja hadi milioni mbili ambazo alizitumia kwa anasa tu.

Hata hivyo mke wa mganga huyo Debora Mwandu(30) amesema kuwa yeye anamshukuru Mungu kwa maisha mapya ndani ya Yesu kwani mganga ambaye ni mume wake aliacha kazi yake ya ufundi wa kushona nguo akidai hapati faida yoyote na kujiingiza kwenye uganga akidai kuwa mizimu imemwambia huko ndiko kwenye mafanikio.

Pamoja na kufanya kazi hiyo kwa miaka saba hakuwahi kununua uwanja wa kujenga nyumba wala kuweka akiba benki huku mambo yao yakienda mrama kutokana na mapato najisi ambapo wateja wake wengi walikuwa ni wahalifu wakiwemo majambazi ambao walikuwa wakiomba dawa ili wafanikiwe katika uhalifu.

Baadhi ya wateja walikuwa wanandoa,wanasiasa na wafanyabiashara ambao walikuwa wakihitaji dawa kwa ajili kuboresha biashara zao lakini alijua kuwa huo ulikuwa ni utapeli ambao ulikuwa unamkosanisha na Mungu.

Hata hivyo katika kazi hiyo mganga huyo alikutana na changamoto kutoka kwa walimu wake ambao walidai kuwa ili kuongeza umaarufu ni vema kutumia viungo vya bindamu hali iliyomkosesha amani kutokana na mauaji ya banadamu jambo ambalo amepingana nalo na kuamua kumwishia Yesu.

Vitendo hivyo pia viliendana na matumizi ya wanyama pori ambazo ni nyara za Serikali  kama mafuta ya Simba au ngozi za wanyama hali ambayo aliona ni hatari kwa maisha yake kwani wakati wowote angeweza kukumbana na mkono wa sheria.

Mganga huyo ametoa wito kwa waganga wa kienyeji kuachana na kazi hiyo kwani haina tija kwa jamii pia huleta uchonganishi kwa jamii na kusababisha mauaji  yasiyo ya lazima kwa jamii isiyo na hatia wakiwamo walemavu wa ngozi.

Aidha ametoa rai kwa wananchi kwamba hivi sasa waganga hao wamenda mbali zaidi kwa kudai kujihusisha na mtandao wa free mason kwa kudai kuwaondolea umaskini watu huku wakiwatoza fedha nyingi na wananchi wengi hutapeliwa kwa matumaini ya kupata utajiri.

Kwa upande wake Mchungaji Laiser wa Kanisa la nyumba ya maombi amesema ujio wa mganga huyo ni kufuatia mfungo wa mwezi mzima ukiokuwepo kanisani kwake hivi karibuni,aidha amesema Kanisa lina mpango wa kumnunulia cherehani ili aendelee kushona  aweze kujikimu kimaisha.

Mussa Shija alimaliza kwa kutoa wito kwa waganga wa kienyeji kuachana na mila potofu za uchonganishi kwa jamii ili kuleta amani katika jamii,Mkoa na Taifa kwa ujumla.





















 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger